• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

BARAZA LA MADIWANI KIBITI LAWAKUMBUSHA WATUMISHI KUWA NA NIDHAMU KAZINI.

Posted on: August 17th, 2024

16.08.2024

Mwenyekiti wa Baraza la Wahe. Madiwani wa Halmshauri ya Wilaya ya Kibiti Mhe. Ramadhan Mpendu amewataka wakazi wa kibiti kutumia vizuri msimu huu wa korosho kupulizia mashamba yao kwa umakini kwa kutumia pembejeo za ruzuku  ambazo Mhe. Rais amezitoa sambamba na kuendelea kuitunza mikorosho hiyo ambayo ni moja ya zao la kiuchumi Wilayani humo.

Pamoja na changamoto ya mvua za msimu uliopita kuathiri mikorosho amewasisitiza wakulima kupitia na kukagua mashamba yao na kuwajulisha maafisa ugani endapo kuna shida huku akimsihi Mkurugenzi Mtendaji kusimamia suala hilo kupitia wataalam wake.

Mhe. Mpendu amesema hayo alipokuwa akifungua mkutano wa BARAZA la Wahe. Madiwani uliofanyika August 15, 2024 katika ukumbi wa Halmashauri hiyo, kwa lengo la kujadili na kupokea taarifa mbalimbali za robo ya 4 kwa mwaka wa fedha 2023/24.

Mbali na kupokea taarifa kwa upande wa masuala ya kiutumishi Baraza limeridhia  shauri la Mtumishi mmoja ambaye ni Afisa Elimu Kata ya Mchukwi Mwl. Martine Peter Benjamin kukatwa mshahara kwa 15% kwa muda wa miaka 3 kwa utovu wa nidhamu, kutokana na utoro wa kutofika ofisini kwa zaidi ya siku 5.

Uamuzi huo umepitishwa baada ya mhusika kukutwa na hatia kupitia kanuni ya 42 (1) ambacho adhabu yake ni kufukuzwa kazi, kushushwa cheo na kupunguziwa mshahara au kukatwa mshahara kwa 15% kwa muda wa miaka 3 mfululizo. Hivyo baraza limewataka Watumishi wote kutii sheria kwa kadri inavyotakiwa kwani maamuzi kama haya huwa hayafurahishi.

Kwa upande mwingine Baraza limepongeza na kutoa ushauri kwa Taasisi za TARURA, RUWASA na TANESCO kwa jitihada zao za kufikisha huduma kwa jamii huku wakisisitiza huduma hizo zifike maeneo yote kwa wakati.

Mara baada ya ufunguzi  Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo alitoa Salam za Serikali akisema Kibiti ni salama changamoto  iliyokuwepo ya wakulima na wafugaji tayari wameshaanza oparesheni ya kutatua mgogoro huo.

Katika kutatua changamoto hiyo Kanali Kolombo ameliomba Baraza la Madiwani kuridhia utoaji wa hati za kimila kwa wafugaji waliotambuliwa ili waweze kuendeleza vitalu watakavyogawiwa. 

Hata hivyo Mkuu huyo wa Wilaya aliainisha kuwa, mpaka sasa tayari vitalu 107 vimeshapimwa kati ya hivyo vitalu 10 ni vya Kijiji cha Uchembe na vilivyosalia ni vya Mtunda na Muyuyu tayari kwa kutekeleza agizo la Mhe. Rais SSH la kuanzisha Ranchi ndogo.

Aidha kutokana na uchache wa mavuno ya mazao ya chakula, Mkuu wa Wilaya aliwasihi Waheshimiwa Madiwani kuwasisitiza wananchi kulima mazao ya chakula zaidi ili Wilaya iweze kuzalisha na kuwa na chakula cha kutosha.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.