• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

BARAZA LA WAHE. MADIWANI LAPITISHA HESABU ZA HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI ZA KUFUNGA MWAKA FEDHA 2023/2024.

Posted on: September 2nd, 2024

Baraza maaluum la Wahe. Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti limeketi tarehe 30.08.2024 ili kupitia na kuridhia hesabu za Halmashauri hiyo za kufunga mwaka wa fedha 2023/2024.

Wajumbe wote kwa pamoja wameridhia hesabu hizo kama zilivyoandaliwa na kuwasilishwa na Mweka Hazina wa Halmashauri hiyo Ndg. Theonest Kibuga, kwani hazikuonekana kuwa na dosari yeyote.

Akizungumza kwaniaba ya Mkuu wa Wilaya, Katibu Tawala Wilaya ya Kibiti Bi. Maria Katemana aliwapongeza Wajumbe kwa kikao kizuri, kazi wanazofanya pamoja na kuridhia taarifa iliyowasilishwa kwenye kikao hicho, huku akitoa pongezi nyingi zaidi Wataalam kwa kazi kubwa waliyofanya ya uandaaji hesabu hizo kisha akatoa maagizo ya Mkuu wa Wilaya:

“Mkuu wa Wilaya ameniagiza niwaambie kama tulivyoona kuna tahadhari zimetolewa na mamlaka ya hali ya hewa nchini kuwa mvua za mwaka huu zinaweza kuwa za wastani au chini ya wastani basi tuhimize sana wakulima watumie vizuri mazao ya chakula waliyo nayo na pia walime yale mazao ambayo yanastawi kwa muda mfupi na yale yanayostahimili ukame”.

“Mhe. DC ameagiza pia wakulima wa mbaazi ambao tayari wamekwishaanza kuvuna wasiuze zao hilo kiholela, wahakikishe zao hilo linauzwa kwa utaratibu kama mazao mengine kwa kupeleka kwenye vyama vyao vya msingi kisha kupelekwa katika ghala kuu kwaajili ya kufanyiwa mnada kama ilivyoagizwa na Serikali” Alisema Bi. Katemana. 

Aidha Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kibiti Mhe. Juma Ndaruke akahitimisha kuchangia hoja kwenye kikao hicho kwa kutoa pongezi nyingi kwa Wahe. Madiwani pamoja na Wataalam kwa maandalizi na mjadala mzuri.

“Kipekee nikupongeze Mhe. Mwenyekiti wa baraza pamoja na Madiwani wako bila kuwasahau Wataalam wetu kwani namna ambavyo taarifa hii imeandaliwa na kuwasilishwa inadhihirisha wazi kabisa kuwa kazi nzuri imefanyika katika Wilaya yetu. Sisi kama chama tutaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Serikali yetu kuhakikisha kwamba lile ambalo tumewagiza mnaenda kulitekeleza katika maeneo mbalimbali na kuturahisishia uchaguzi huko tunakoenda” Alisema Mhe. Ndaruke.

Mwisho, Mwenyekiti wa baraza la hilo Mhe. Ramadhani Mpendu akafunga kikao hicho kwa kuwataka Wahe. Madiwani, Mkurugenzi pamoja na Wataalam kutobweteka na pongezi zilizotolewa kwao, badala yake waendelee kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha kila kitu kipo kwenye utaratibu wake ili miaka ijayo mambo yawe vizuri zaidi.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • UTEKELEZAJI WA KAMPENI YA TAIFA YA CHANJO WAANZA WILAYANI KIBITI.

    June 30, 2025
  • NYAMATANGA YAKABIDHIWA GARI JIPYA LA WAGONJWA.

    June 27, 2025
  • KANALI KOLOMBO:SERIKALI INATAMBUA MCHANGO WA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI

    June 12, 2025
  • PPRA KANDA YA PWANI YATOA MAFUNZO KUHUSU SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA NA MFUMO WA KIELEKTRONIKI WA UNUNUZI WA UMMA

    June 12, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.