• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

BOT YAWANOA WATUMISHI WA UMMA NA WAFANYABIASHA KIBITI JUU YA UTAMBUZI WA ALAMA NA UTUZANJI BORA WA FEDHA.

Posted on: December 22nd, 2022


Benki Kuu ya Tanzania (BOT) tawi la Dar es Salaam imetoa mafunzo kwa watumishi wa umma na wafanyabiashara wa Wilaya ya kibiti juu ya utunzaji bora wa fedha na namna ya kutambua alama zilizopo  ikiwa ni utaratibu wa kawaida nchini kadri bajeti itakavyoruhusu ambapo wameanza na Mkoa wa Pwani.

Akitoa Elimu kwa nyakati tofauti  katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri na stendi kuu ya mabasi Kibiti, Mkuu wa msafara Restituta Minja kitengo cha sarafu amesema ,fedha zinatakiwa kuhifadhiwa katika bahasha au pochi ili kuepuka zisijikunje na kuchanika  kwani uchakavu wa fedha  huisababishia serikali  hasara kubwa kwa sababu fedha mbovu zote huchambuliwa na kuharibiwa.

Vilevile Minja amesisitiza kuwa fedha zihifadhiwe katika maeneo safi na makavu na ili zisijikunje ni  muhimu kuwa na pochi (wallet) imara au kasha la kuhifadhia ,sarafu na noti pia sambamba na kuzihifadhi katika  maeneo yasiyo na vumbi kemikali au vyombo vinavyotoa rangi ambapo si rahisi moto,maji ,wadudu na wanyama kufikika kwa urahisi kwani fedha kwa asilimia 100 hutengenezwa na pamba na ni rahisi kuharibika au kuteketea.

Hata hivyo amekemea utunzaji mbaya wa fedha kama vile kufinyanga noti au kuikunja mkononi,kuweka noti au sarafu kwenye soksi au chini ya godoro,kuweka fedha kwenye uchafu na unyevunyevu,kuhifadhi fedha kwenye nguo za ndani au kufunga katika pindo ya kitenge au kanga hasa kina Mama ambao pia huifadhi kwenye maziwa na kuchimbia noti au sarafu aridhini utunzaji huo haustahili kutumia .

Katika hatua nyingine Minja amesema kila mwananchi anajukumu la kujua alama za fedha ili aweze kuzitambua panapotokea changamoto ya fedha feki na utapeli huku akisisitiza wafanyabiashara kuepuka kupokea fedha taslimu kwani ni chanzo cha kupokea fedha feki kwa kuchanganywa na fedha salama na halali.

Alama za kiusalama kwenye fedha hutambulika kwa njia tatu ambazo ni kwa njia ya macho kwa kusaidiwa na mwanga,kwa njia ya kuhisia na kwa njia ya tochi maalum ambayo ni kifaa maalum (uv tortch.)hususani katika eneo lenye giza huonyesha baadhi  ya alama zilizojificha .

Aidha Mwezeshaji Minja amesema Tanzania haina kiwanda cha kutengeneza fedha hivyo zoezi hilo hukamilika kwa kutoa zabuni,nje ya nchi ,na ufanyika kwa ushirikiano na usiri mkubwa.Pia benki kuu imeunda sera ambayo itamwezesha mtanzania yeyote kufika benki iliyo karibu kubadilishiwa fedha zilizochakaa kwa utaratibu maalum Kwa maelekezo kutoka BOT ikiwa ni pamoja na sarafu zilizochakaa.

“Kutokana na uwepo wa alama mbalimbali kwenye fedha,ifike wakati serikali iwe na mzabuni mmoja wa kutengeneza pesa hizo ili kuepuka kuwa na alama nyingi”alisema mfanyabiashara  aliyewakilisha wananchi wa kibiti

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya na watumishi wa umma Katibu Tawala wa Wilaya Milongo Sanga ameipongeza Benki Kuu kwa kutoa mafunzo ya Elimu ya uhifadhi na utambuzi wa fedha,na anaimani kubwa wananchi na watumishi wameelewa pia ametoa wito kwenye mabenki kusitisha kutoa fedha zilizochakaa na elimu hiyo kuwa endelevu.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Mohamed Mavura alitambulisha ugeni kutoka benki Kuu na kuwataka watumishi kusikiliza kwa makini kwani mafunzo hayo ni ya muhimu katika maisha ya kila siku.

Mara baada ya Mafunzo kukamilika Afisa Biashara wa Wilaya Sadelick Kihongosi ameishukuru Benki Kuu kwa kutoa mafunzo,mbali na kuwafundisha watumishi wa umma na wafanyabiashara Elimu ya utambuzi na uhifadhi bora wa fedha ni muhimu kwa wananchi wote kutokana na shughuli mbalimbali za kibinadamu .


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.