• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

DC KIBITI AKABIDHI GARI LA WAGONJWA KWA IDARA YA AFYA NA VISHKWAMBI KWA IDARA YA KILIMO.

Posted on: December 1st, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amekabidhi gari la wagonjwa lililotolewa na Wizara ya Afya na vishkwambi 17 kwa maafisa ugani wa Idara ya Kilimo vilivyotolewa na Wizara ya kilimo.

Akikabidhi gari hilo la wagonjwa (ambulance) linalokwenda kuhudumia katika kituo cha Afya Mbwera Kanali Kolombo amesema gari hilo ni neema  kwani linakwenda kuokoa maisha ya wakazi wa Mbwera na maeneo ya jirani licha ya kuwa bado kuna uhitauhitaji wa magari hayo katika vituo vya afya vilivyosalia.

"Licha ya kuwa Bado tunaupungufu wa magari hayo katika vituo vingine vitatu, kwa niaba ya wakazi wa Kibiti ninaishukuru Serikali ya Mama Samia kwa kutujali" Alisema Kanali Kolombo.

Vilevile Kanali Kolombo amekabidhi vishkwambi 17 kwa maafisa Ugani, huku akisema vinakwenda kurahisisha kazi za kitakwimu katika ngazi ya wilaya na kuanza kufanya kilimo cha ushindani katika kila kata.

"Kwa Afisa ugani ambaye kata yake itashindwa kuwa na mapato ya kutosha, nitakuwa na maswali ya kumuuliza" Alisema Kolombo.

"Kilimo ni Uti wa mgongo wa uchumi wa Kibiti, Serikali imetuwezesha vishkwambi hivi ambavyo ni kipimo tosha natarajia kuona Idara ya Kilimo inakuwa na takwimu sahihi za mazao mbalimbali wakati wote." Alisema Kanali Kolombo.

Naye Mbunge wa Jimbo la kibiti Mhe. Twaha Mpembenwe mbali na pongezi amesema ni furaha kupata gari la wagonjwa Mbwera na anakwenda kulikabidhi rasmi kwa hafla maalum. Pia Mhe. Mpembenwe amewataka maafisa ugani wote waliopokea vishkwambi, kuvitumia kwa malengo yaliyokusudiwa na si vinginevyo.

Aidha akisoma taarifa ya mapokezi hayo Mganga Mkuu wa Wilaya Dr. Elizabeth Oming'o amemshukuru Mhe SSH na Mbunge wa Kibiti kwa kuwathamini wakazi wa Kibiti kwa kuwapatia gari hilo kwani  linakwenda kurahisisha utoaji wa huduma katika Sekta ya Afya hususani maeneo ya delta na kupunguza vifo vya kina mama wajawazito na watoto wachanga.

Hafla hiyo imefanyika katika viunga vya Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti na kushuhudiwa na Mhe. Mbunge wa Jimbo la Kibiti Mhe. Twaha Mpembenwe, Madiwani wa Halmshauri ya Wilaya ya Kibiti, Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na watumishi wa Halmashauri hiyo tarehe 30.11.2023

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.