• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

DED KIBITI ALONGA NA WATUMISHI IDARA YA AFYA.

Posted on: January 5th, 2023

DED KIBITI ALONGA NA WATUMISHI IDARA YA AFYA.

ASISITIZA NIDHAMU NA UTII KUWA NGUZO YA UWAJIBIKAJI.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya kibiti Mohamed Mavura amewaagiza watumishi wa Idara ya Afya kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia taratibu na kanuni za kazi ili kuweza kuihudumia jamii inayowazunguka ipasavyo.

Amesema hayo alipokuwa katika kituo cha Afya Kibiti ikiwa ni kikao cha kawaida cha utendaji ambapo amewaonya na kuwataka  watumishi kuwa na matamshi yenye lugha nzuri kwa wateja (jamii) pindi wanapowapokea na kuwahudumia huku akisisitiza madaktari na manesi (senior) wazoefu, kuwaelekeza vijana hao (Juniors) namna ya kufanya kazi na kuwasiliana na jamii wanayoihudumia.

“Kila mmoja afanye kazi kwa kufuata taratibu na kanuni kwa kuzingatia miiko ya kazi,sitaweza kuvumilia mtumishi ambaye hana nidhamu kazini” alisema Mavura.

Vilevile Mavura amewataka watumishi wote wa Idara hiyo  kuheshimu Uongozi uliopo madarakani, kukubali mabadiliko yaliyopo na kuwa tayari kuendana nayo ili kuhakikisha kazi zinakwenda kama kanuni zinavyoelekeza ikiwa ni pamoja na kufanya kazi kwa kushirikiana (team work).

“ Vunjeni makundi yanaharibu kazi ,heshimuni mamlaka iliyopo madarakani na kuitii huo ndio utumishi wa UMMA”alisema Mavura.

Hata Hivyo Mavura mbali na kumpongeza Mganga Mfawidji wa kituo hicho Dr Beatrice pia amemuagiza  kuongeza kasi ya  utendaji kwani kituo hicho katika ngazi ya Wilaya kinategemewa na wateja wengi kwa ajili ya huduma za kitabibu hivyo anahitaji maboresho yenye kuleta mtazamo chanya kiutendaji.Pia Mkurugenzi Mavura amemuagiza Daktari huyo kuhakikisha anasimamia ukusanyaji mapato katika Idara hiyo na Kupeleka bank Kwa usalama zaidi fedha zilizopatikana Ili baadae ziweze kuisaidia kukamilisha miradi maendeleo inayoendelea.

Daktari Beatrice Malekela anachukua nafasi ya Daktari Sospeter Eunda ambaye kwa sasa ni Daktari wa kawaida katika kituo hicho, ameachia nafasi hiyo baada ya kuomba kupumzika kutokana na changamoto za kiafya zinazomkabili

Daktari Sospeter ambaye kabla ya kuwa Mganga Mfawidhi  alikuwa Daktari wa kawaida kituoni hapo, mbele ya watumishi wa Idara ya afya, Mkurugenzi Mtendaji na Mganga Mkuu wa Wilaya, amewasihi watumishi hao kumpa ushirikiano Daktari Beatrice ambaye ni Mganga Mfawidhi rasmi kama walivyokua wakishirikiana nae kwani yeye kwa sasa atakuwa Daktari wa kawaida na kazi ziendelee.

“Kwa muda niliokuwa kiongozi ,nimefanya kazi kadri nilivyoweza na sasa nimeachia madaraka huku nikiendelea kuihudumia jamii katika taaluma yangu ya udaktari,tuko pamoja kiutendaji, naomba mumpe Dr Bearice ushirikiano ili tuweze kutimiza wajibu wa  kuwatumikia wananchi” alisema Daktari Sospeter.

Awali Mganga Mkuu wa Wilaya Daktari Elizabeth Oming’o akimkaribisha Mkurugenzi kuongea na watumishi alisema Kituo cha Afya Kibiti ni Kituo muhimu Kwa kutoa huduma za Afya,yeye na timu yake wanaendelea kupambana kuhakikisha huduma zote muhimu zinapatikana ikiwa ni pamoja na kusimamia miradi kikamilifu na mpaka sasa katika kituo hicho wanajenga Jengo la upasuaji ambalo kwa sasa liko katika hatua ya jamvi lengo likiwa ni kutanua na kuboresha huduma za  Afya katika kituo hicho.Mwisho amelishukuru shirika la KOFFIH International kwa namna linavyokuwa mstari wa mbele kuhakikisha kituo hicho kinaboresha huduma kwa kutoa michango mbalimbali ya maendeleo.

Aidha Mganga Mfawidhi Daktari Beatrice Malekela amesema,Kwa upande wa Mapato katika kituo hicho  wanatarajia kukusanya mil 10 kwa mwezi kuanzia sasa wakati huo huo akamshukuru Mkurugenzi kwa kuwatembelea huku akisema maagizo na maelekezo ameyapokea na anakwenda kutekeleza kwa kuyafanyia kazi .



Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.