• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KANALI KILOMBO: WADAU JITOKEZENI KUWASAAIDIA WAHANGA WA MAFURIKO KIBITI. KAMBI YA SHIMO LA HELA YAFUNGWA RASMI, MISAADA YOTE KUTOLEWA KAMBI YA KITUMBINI.

Posted on: April 14th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo akiwa ameambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama, amepaza sauti akiwasihi wadau mbalimbali kujitokeza kuwasaidia wahanga wa Mafuriko Wilayani humo ambao kwa kiasi kikubwa hawana makazi na vyakula baada ya nyumba zao kuzingirwa na Maji na mazao kusombwa kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.

"Wadau mbalimbali,Taasisi na watu binafsi popote mlipo naomba muitizame Kibiti kwa jicho la tatu, wahanga hawa wanauhitaji mkubwa, hali si shwari kwa sasa" Alisema Kolombo.

Akizungumza kwa msisitizo Kanali  ameeleza kuwa ndani ya Wilaya ya Kibiti vijiji 19 vinapatikana katika delta ya Rufiji,  ambapo tayari maji ya  Mafuriko hayo yamefika katika vijiji hivyo.

"Mpaka sasa tuna jumla ya wahanga 36,900 ambapo mbali na nyumba zao kufikiwa na maji wapo pia wahanga ambao mashamba yao yameharibiwa kabisa na maji tumeorodhesha wote" Alisema.

Kanali Kolombo amebainisha hayo Jana alipokuwa katika ziara muhimu yenye lengo Kuangalia Usalama wa kambi na afya za binadamu, Kukabidhi misaada iliyotolewa kwa wahanga, Kukagua njia zinazotumika kufikisha misaada, Kuangalia ukubwa wa janga na kukagua namna kambi zinavyopokea wahanga hao.

Mara baada ya kujiridhisha Mkuu huyo wa Wilaya ameifunga kambi ya shimo la Hela rasmi kwa sababu tayari imekwishazingukwa na maji  na kuamuru wakazi wote kuhamia kambi ya Kitumbini ambapo ni salama zaidi na misaada itatolewa huko.

"Kuanzia sasa kambi hii naivunja hameni, kambi itakayotumika ni ya Kitumbini na misaada yote itatolewa huko na si kwingineko" Alisema.

Kanali Kolombo amewasihi wananchi kuishi kwa utulivu na kufuata maelekezo huku akiagiza Kuimarishwa kwa ulinzi na kufunguliwa kwa zahanati Kambini hapo kwa ajili ya huduma za kiafya n.k. Pia ameiagiza TARURA kuhakikisha kwa namna yeyote wanafungua Barabara ya kikale mpaka Mtunda ili iweze kurahisisha usafirishaji wa misaada sambamba kuhakikisha chakula kinagawiwa kwa walengwa na si vinginevyo pamoja na misaada mingine.

Licha ya maagizo hayo  Kanali Kolombo amewataka wakazi wote wanaoishi maeneo ya delta na mabondeni kuendelea kuhama kwa haraka  kuelekea maeneo yaliyoinuka na kwenye makambi kwani mvua bado zinatarajiwa kuendelea kunyesha kwa wingi.


"Kwa mujibu wa Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania, mvua zitaendelea kunyesha hadi mwezi mei  endeleeni kuhama kuelekea kwenye kambi zilizotengwa hususani maeneo ya miinuko" Alisema Kanali Kolombo.


"Misaada yote itatolewa kwenye makambi niwasihi tu elekeeni kwenye kambi muweze kupata huduma, hususani kambi zilizotengwa za kitumbini, kikwajuni, mtomboli na Mkwinda" Alisema.

Akigawa misaada hiyo Kanali Kolombo ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu Menejimenti ya Kitengo cha Maafa, na Mdau mmoja Dr. Alice Kaijage kwa kuwajali wananchi na  kuwaletea misaada mbalimbali ambayo tayari  imeshaanza kusambazwa na mingine inaendelea kusambazwa kwa wahanga.


Aidha Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kibiti SSP John Mwakalukwa akitoa Salam za pole amewataka wote wenye vitendo viovu Kambini hapo kuacha mara moja kwani jeshi la Polisi limejipanga vizuri kukabiliana na wote wenye nia ovu Kambini hapo.

Naye Inspekta Fransisco Chunji akimwakilisha kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani kutoka kikosi cha uokoaji katika Salam zake za pole amewasihi wananchi hao kuthamini maisha yao kwa kuishi kwa tahadhali kubwa na kufuata maelekezo watakayopewa na viongozi pamoja na wataalam ili kuweza kujinusuru pamoja na watoto.

Nao baadhi ya wazee wananchi wameishukuru Serikali na Mdau kwa kuwajali katika kipindi hiki, wameishukuru Kamati ya Ulinzi na Usalama kwa kuwasimamia vema na kuwafikia makabini, huku wakikiri kuwa tayari kutoka katika maeneo hayo endapo wakipewa makazi ya kudumu. Mbali na hayo wameomba kupatiwa huduma za kiafya, usafiri, maji safi na salama, vyakula, malazi na mbegu za muda mfupi ili waweze  kuanza kulima upya.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KANALI KOLOMBO:SERIKALI INATAMBUA MCHANGO WA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI

    June 12, 2025
  • PPRA KANDA YA PWANI YATOA MAFUNZO KUHUSU SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA NA MFUMO WA KIELEKTRONIKI WA UNUNUZI WA UMMA

    June 12, 2025
  • KANALI KOLOMBO AIPONGEZA MARINE PARKS KUANZISHA MIUNDOMBINU YA KUHIFADHI NA KULINDA MATUMBAWE BAHARINI

    May 10, 2025
  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.