• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KANALI KOLOMBO AFUNGUA MAFUNZO YA UONGOZI KWA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA WILAYANI KIBITI.

Posted on: December 13th, 2023

12.12.2023

Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amefungua mafunzo ya siku tatu ( 12-14 Disemba,) ya Uongozi, usimamizi pamoja na uanzishwaji wa jumuiya za kujifunza mashuleni (JzK) yakiendeshwa na wakufunzi /wawezeshaji watatu kutoka chuo cha Uongozi ADEM Bagamoyo na Mwanza, Mratibu wa shule Bora wa Mkoa wa Pwani Bi. Oliver kapaya, mwakilishi kutoka Ofisi ya uthibiti ubora wa shule na Afisa Taaluma msaidizi Idara ya Elimu Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Mwl. Violeth Mahimbo.

Washiriki mafunzo hayo  ni Maafisa Elimu Kata, Walimu Wakuu wote wa shule za msingi na  Viongozi wa ngazi ya Halmashauri ambao walitangulia kushiriki mafunzo tarehe 11/12/2023.

Mafunzo hayo ni mpango mkakati wenye lengo kuwajengea uwezo Viongozi kwenye masuala ya Uongozi na usimamizi Bora uliokusudiwa kuimarisha ufundishaji na Ujifunzaji.

Akimkaribisha Mkuu wa Wilaya, Katibu Tawala wa Wilaya Bi. Maria Katemana amesema anaamini baada ya mafunzo haya, washiriki wote watakwenda kupanga na kusimamia wenzao kujitathmini ili waweze kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Aidha akifungua mafunzo hayo katika ukumbi wa shule ya wavulana Kibiti Kanali Kolombo amesema kuwa, Mtaala wa Elimu ya Msingi uliowekwa na dira ya Serikali umelenga kumuandaa Mtanzania kuwa na mtazamo chanya unaothamini usawa na elimu bila ukomo.

"Ninawashukuru walimu kwa kuitikia wito wa kushiriki na kupokea mafunzo haya hongereni sana huu ni mpango wa Mhe. Rais tunamshukuru sana".

Hata hivyo, Kanali Kolombo aliendelea kusema kuwa,  licha ya matokeo ya Kibiti kutoridhisha ni wakati sahihi sasa kupitia mafunzo hayo ya uongozi kutafuta mbinu mbadala na  kuongeza jitihada ili kuweza kupiga hatua zaidi.

Naye Mwl Iddi Ally, Afisa Elimu Kata wa Kata ya Mlanzi ambaye ni mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo amesema, mafunzo waliyopitishwa yamejikita zaidi kwenye kuongeza maarifa na mbinu za usimamizi wa jumuiya za kujifunza ( JzK) .

Vilevile Mwl. Iddi Ally amesema kupitia mafunzo hayo wamewezeshwa kujua umuhimu wa kujifunza, na ya kuunda muundo wa jumuiya hizo kwa ngazi za shule .

Halikadhalika amesema, kuwezeshwa kujua manufaa ya JzK katika kutatatua changamoto zinazokwamisha ujifunzaji na ufundishaji ni jambo ambalo liko ndani ya uwezo wa shule na Kata kwa ujumla.

Akifafanua kuhusu shule Bora Mratibu wa shule Bora Bi. Oliver Kapaya alisema shule Bora ni mpango na mradi wa Serikali unaofadhiliwa na Serikali ya Uingereza kupitia mfuko wa UKAID unao lenga kuinua kiwango cha elimu ya Awali na Msingi nchini. Program ya Shule Bora inatekelezwa katika Mikoa Tisa Tanzania Bara.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.