• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KANALI KOLOMBO AFUNGUA MNADA WA KOROSHO MKOA WA PWANI.

Posted on: November 1st, 2023

Mnada wa kwanza wa korosho msimu wa 2023 Mkoa wa Pwani umefunguliwa rasmi wilayani Kibiti Leo novemba mosi ukiwa na wazabuni 27  ambapo korosho zimeuzwa Kwa bei ya wastani ya sh.  2094.46 kwa daraja la kwanza na sh 1600 kwa daraja la  pili baada ya wakulima wote kukubaliana kuuza kwa bei hiyo.

Katika mnada huo  jumla kilogram 3,711,235  za korosho  zilizouzwa ni za daraja la kwanza na kilogram 146,372 ni za daraja la pili.

Akizungumzia tozo zinazowahusu wakulima katika ngazi ya kimkoa na kitaifa Meneja wa COREKU Mkoa wa Pwani Hamis Mantawela  amefafanua kuwa, jumla ya makato ya tozo ni 208.94 ambapo tozo ya uendeshaaji wa vyama vya ushirika ni sh. 100, tozo ya Halmshauri ni sh. 56.94, tozo ya Bodi ya korosho ni sh 25, tozo ya Tali Naliendele ni sh 25, tozo ya wadau ni sh 2 wakati tozo ya usafiri hutegemea na umbali wa Amcos.

Akifungua mnada huo Mkuu wa Wilaya ya Kibiti na Mgeni rasmi Kanali Joseph Kolombo amewaagiza wakulima vyama vya ushirika kuhakikisha wanazuia utoroshaji wa korosho ndani ya Wilaya husika, vyama vya Msingi kutoa elimu kwa wakulima na kuhakikisha havipokei korosho mbichi.

"Kwa yeyote atakaekamatwa akitorosha korosho, chombo chake Cha usafiri na mzigo wake vitataifishwa" Alisema Kanali Kolombo.

Hata hivyo amewataka wanunuzi  na Taasisi za fedha kuwalipa haraka na kwa wakati wakulima ili waweze kufanya mambo yao ya maendeleo huku akisisitiza wakulima hao kuhakikisha Katika msimu huu wa mvua wanalima mazao ya chakula pia.

"Nataka katika msimu huu kila kaya kuwa na hekari nne za mazao ya chakula Wilaya ya kibiti sambamba na mazao mengine ya biashara kama vile mbaazi na nitakagua. "Alisema Kolombo.

Vilevile Meneja wa Tawi la Dar es Salam Bodi ya korosho Bi. Domina Mkangara, ametoa Rai kwa wakulima wote kuhakikisha wanaokota korosho kila siku mashambani ili kuhakikisha  zinakauka vizuri na kuwa katika  ubora unaotakiwa katika kipindi hiki ambacho mvua zimeanza kunyesha.

Aidha kwa niaba ya Msajili wa Vyama vya ushirika Bw. Hamas Chacha amesema, Msajili ameagiza wakulima wote kupeleka kwa wakati korosho kwenye maghala yaliyoainishwa, pia amewaelekeza viongozi wa vyama vya Msingi kushughulikia masuala ya minada mapema huku akikitaka Chama Kikuu kuhakikisha kinasimamia malipo ya wakulima ndani ya siku Saba.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.