• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KANALI KOLOMBO AKAGUA MIRADI YA MAJI KIBITI.

Posted on: February 27th, 2023

Katika kuhakikisha Miradi miradi inajengwa kwa viwango, na inakamilika kwa wakati , Kamati ya ulinzi na usalama  Wilaya ya Kibiti ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya Kanali Joseph Kolombo imetembelea na kukagua miradi 5 ya maji  inayotekelezwa ndani ya Wilaya kupitia wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini RUWASA yenye dhamira ya kupunguza tatizo la uhaba wa maji kwa kiasi kikubwa mara tu itakapokamilika.

Katika ziara hiyo kamati iliwasili  Kijiji cha Mjawa, ambapo walikagua mradi wa maji ya bomba wenye thamani ya sh 503,600,761.96 unaotekelezwa kwa fedha za mfuko wa maji wa Taifa (NWF) chini ya Mkandarasi M/s Trinity manufacturing services Ltd, na ujenzi umekamilika kwa 80%. Katika mradi huu kunajengwa  mnara wa mita 12 utakaobeba tanki la maji lenye ujazo wa Lita 150,000 (150M3) na kazi inaendelea.

Mradi wa maji Mjawa

 

Vilevile walikagua mradi wa maji ya bomba wa Mahege wenye thamani ya sh 383,290,130,80 unaotekelezwa kwa fedha za Uviko 19 kwa usimamizi wa Mkandarasi FEDERICK CONSTRUCTION COMPONY LTD na mpaka sasa umekamilika kwa 90% na kazi zinaendelea. Katika mradi huu pamejengwa mnara  wa mita 9 wa tanki la maji lenye ujazo wa Lita 50,000 huku ukitarajiwa kuwafikia wakazi wapatao 2731 .

Mradi wa maji Mahege

 

Wakiwa katika Kijiji cha mchungu ambapo pia walikagua mradi wa maji ya bomba wenye thamani ya sh 452,660,782.35  kwa fedha za mfuko wa maji wa Taifa (NWF) na kusimamia na  Mkandarasi wa M/S FEDERICK CONSTRUCTION COMPANY Ltd, ambao ukikamilika utasaidia kunufaisha wananchi wapatao 1220. Katika mradi huu kunajengwa mnara wa  mita 12 na tanki la maji lenye ujazo wa Lita 50,000 ujenzi upo hatua ya umaliziaji.

Pia walitembelea mradi wa maji wa Kilulatambwe wenye thamani ya sh 790,116,495,00 chini ya Mkandarasi M/S Ecia kwa fedha za mfuko wa maji wa Taifa (NWF) na kukamilika kwa ujenzi huu kutanufaisha wananchi wapatao 1033. Katika Mradi huu kunajengwa mnara wa mita 6 na tanki lenye ujazo wa Lita 50,000.

Mradi wa maji Kilulatambwe

Mwisho ziara ikahitimishwa katika Kijiji cha Mtunda penye mradi mkubwa kupita yote ambapo hujengwa tanki la maji lenye ujazo wa lita 200,000 juu ya mnara wa mita 12, wenye thamani ya sh 790,116,495.00 chini ya Mkandarasi M/S Ungando & General supplies Ltd ukitarajiwa kunufaisha wakazi wapatao 7476 katika Kijiji cha Mtunda A na B .

Mradi wa maji Mtunda

Katika miradi hiyo licha ya kujenga minara na matanki ya maji pia kunajengwa ofisi, nyumba za watumishi, vituo vya kuchotea maji, ujenzi wa nyumba za mitambo, uchimbaji wa mitaro, ulazaji na ufunikaji wa mabomba pamoja na ufungaji wa pampu za kusukumia maji.

Aidha, Mkuu wa Wilaya Kanali Joseph Kolombo, amepongeza jitihada zinazoendelea katika miradi hiyo na kuiagiza taasisi ya TANESCO kuhakikisha nishati ya umeme inafika kwa wakati kwenye miradi na kwa upande wa  TARURA kuimarisha miundombinu ya barabara ambayo haiko vizuri ili paweze kupitika na kufikika kwa urahisi. Pia ameagiza kukamilisha hatua zote za umaliziaji wa Miradi zilizobakia kwa wakati huku akiahidi kufuatilia kwa karibu changamoto ya fedha za malipo ya wakandarasi hao.

Naye Meneja wa RUWASA Wilaya ya kibiti Mhandisi Pascal Kibang'ule  amesema ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Kibiti na Kamati ya Ulinzi na usalama kwa ujumla katika Miradi ya Maji, imekuwa chachu ya kuamsha kasi ya utekelezaji wa Miradi ya Maji, hasa kwa  jinsi alivyoonyesha ushirikiano wa kufuatilia madai ya wakandarasi yalipwe kwa wakati, na kuhamasisha utekelezaji wenye  viwango. Vilevile Mhandisi Kibang’ule amesema wana Kibiti watarajie utekelezaji wa Miradi ya Maji yenye viwango, ikiendana na sera ya kumtua mama ndoo kichwani kwa kufikisha asilimia 85 ya upatikanaji wa huduma ya Maji vijijini ifikapo 2025.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KANALI KOLOMBO:SERIKALI INATAMBUA MCHANGO WA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI

    June 12, 2025
  • PPRA KANDA YA PWANI YATOA MAFUNZO KUHUSU SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA NA MFUMO WA KIELEKTRONIKI WA UNUNUZI WA UMMA

    June 12, 2025
  • KANALI KOLOMBO AIPONGEZA MARINE PARKS KUANZISHA MIUNDOMBINU YA KUHIFADHI NA KULINDA MATUMBAWE BAHARINI

    May 10, 2025
  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.