• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KANALI KOLOMBO ATAKA KASI YA UJENZI KUONGEZEKA.

Posted on: June 14th, 2023


NI KATIKA MAENDELEO YA UJENZI WA SHULE MPYA 2 ZA MRADI WA BOOST.


Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo, amefanya ziara ya ufuatiliaji wa maendeleo ya ujenzi wa shule mpya 2 za kisasa, unaotekelezwa na mradi wa Boost Tanzania. Boost ni mradi unaosaidia kuboresha miundombinu ya shule za msingi na awali sambamba na dhana nzima ya ufundishaji na ujifunzaji.


Akitoa majumuisho ya ziara hiyo Mkuu wa Wilaya amewaelekeza Mkurugenzi Mtendaji, Mwenyekiti wa Miradi na Wataalam aliambatana nao, kusimamia kwa weledi mradi huo na kuhakikisha unakamilika kwa viwango na ubora unaotakiwa.

Katika maelekezo hayo pia, Kanali Kolombo amewataka wasimamizi wa miradi kuhakikisha wanawasimamia kikamilifu mafundi ili kuhakikisha wanakuwepo eneo la ujenzi kila siku, Pamoja na kufanya kazi yenye ubora wa hali ya juu ili kuondoa kabisa makosa ya kiufundi, kwani ikiwa mapungufu yatajitokeza hapatakuwa na fedha za nyongeza za kufanya marekebisho.

"Miradi yote isimamiwe kikamilifu, hapatakuwa na fedha za nyongeza, hilo lieleweke hivyo, zaidi ya hapo mtafidia wenyewe".Alisema Kolombo.

Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Ndg. Hemed Magaro amesema maelekezo yote ameyapokea na kuahidi kuyafanyia kazi kwa kushirikiana na wataalamu wake.

Licha ya kutoa pongezi kwa kazi nzuri inayoendelea, Mkurugenzi Magaro ameisisitiza kamati ya ujenzi, wasimamizi na mafundi kuongeza jitihada ya ujenzi kwa kuzingatia ubora na maelekezo ya BOQ.

Vilevile Magaro kwa nyakati tofauti, amemwagiza Afisa Elimu na Mhandisi kuhakikisha katika maeneo yote ya miradi kunakuwa na kitabu cha wageni kusaini, kuwepo na utunzaji wa nyaraka au mikataba, na stoo kwa ajili ya kuhifadhia vifaa vya ujenzi wakati kazi zikiendelea.

Aidha hali ya maendeleo ya ujenzi katika miradi yote 2 iko katika hatua ya kujenga msingi, kuweka kifusi na kumwaga jamvi kwa baadhi ya majengo na kazi zinaendelea.

Katika miradi hiyo jumla ya sh 306, 900,000/= kwa kila shule zimepokelewa ambapo kila shule  kutajengwa madarasa 7, matundu 10 ya vyoo, Jengo la Utawala, kichomea taka, madarasa 2 ya awali yenye matundu 6 ya vyoo pamoja na vifaa vya michezo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.