• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KANALI KOLOMBO AZINDUA ZOEZI LA UCHANJAJI CHANJO YA SURUA NA RUBELLA, ASISISTIZA WAZAZI NA WALEZI KUPEKEKA WATOTO KUPATIWA CHANJO.

Posted on: February 16th, 2024

Zoezi uchanjaji wa chanjo ya SURUA na RUBELLA nchini limezinduliwa tarehe 15/2/2024. Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti kama ilivyo kwa Halmashauri nyingine nchini wametekeleza zoezi hilo katika hospitali ya Wilaya ya Kibiti iliyopo nje kidogo ya mji katika Kata ya Mtawanya.


Mganga Mkuu wa Wilaya Daktari Elizabeth Oming'o amesema chanjo hiyo ni muhimu sana hivyo ni vema kuhakikisha hakuna mtoto atakayekosa chanjo, kwani kwa hali ya kawaida unaweza ukaona haina maana lakini ukaja kupatwa na madhara baadaye.


"Ndg. wananchi, leo tumezindua chanjo hii , zoezi hili linafanyika nchi nzima siku ya leo hivyo msipuuze. Kibiti tutatoa huduma ya chanjo katika vituo vyote vilivyopangwa kuanzia leo tarehe 15 -18, waleteni watoto wapatiwe chanjo" Alisema Dkt. Oming’o. 

Mbali na kutambua umuhimu wa chanjo Mganga huyo amewasisitiza wananchi waliofika kwenye uzinduzi huo, kuwaelimisha na kuwajulisha watu ambao hawakuweza kufika wawapeleke watoto wao wakapatiwe chanjo hiyo.


Vilevile amesema timu za uchanjaji zitakuwa katika vituo vya kudumu, vituo kuhamahama na katika maeneo mbalimbali ikiwemo maeneo ya masoko, shule, nyumba za Ibada, mashambani, vituo vya mabasi, kambi za wakimbizi, kambi za wavuvi na katika maeneo ya mipakani ambapo kuna watoto (transit sites).


Akimkaribisha Mkuu wa Wilaya kuzungumza na halaiki iliyojitokeza katika uzinduzi huo, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kibiti Bi.Maria Katemana amewaagiza wadau wa Afya kuendelea kuwasisitiza kinamama kuwapleka watoto kupata chanjo katika vituo vilivyopangwa kwenye maeneo yao.

Katika uzinduzi huo, Mkuu wa Wilaya ya Kibiti na Mgeni rasmi katika shughuli hiyo Kanali Joseph Kolombo  amesema, Serikali imejiwekea mpango mzuri wa kuhakikisha wananchi wanaishi wakiwa na Afya bora ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa chanjo za kujikinga na magonjwa kama hayo.


Kanali Kolombo amesema, lengo la kuleta chanjo nchini ni kuhakikisha wanaongeza Kinga kwa walengwa kuzuia kuenea kwa magonjwa yanayozuilikia ikiwa ni pamoja na Surua na Rubella.

"Nawasihi wazazi, walezi, baba na mama pelekeni watoto wakapatiwe chanjo, hata sisi enzi zetu tulipata chanjo kama za ndui polio n.k na tuliona mafanikio yake" Alisema Kolombo.

Surua na Rubella  ni magonjwa yanayosababishwa na virusi kwa njia ya hewa. Na dalili za magonjwa hayo nyingi hushabihiana,  kama vile kupatwa na homa Kali, mafua, kikohozi , macho kuwa mekundu yakiambatana na kutoa majimaji, kupatwa na vipele vidogodogo ambavyo huanzia kwenye paji la uso, nyuma ya masikio, kisha kusambaa usoni na mwili mzima.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.