• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KANALI KOLOMBO KUKUTANA NA WAZAZI PAMOJA NA WANAFUNZI WALIOPATA MIMBA NA WATORO, NI KATIKA KIKAO CHA TATHMINI YA ELIMU KIDATO CHA II WILAYANI KIBITI.

Posted on: December 27th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo ameagiza Wakuu wa shule kuwapa taarifa wazazi, walezi na wanafunzi waliopata mimba wakiwa shuleni kuwasili ofisini kwake mwanzoni mwa mwezi January waweze kujadili na kutafuta mwarobaini wa utoro na mimba za utotoni.

"Majina ya wanafunzi wajawazito mnayajua, waandikiwe barua wafike ofisini kwangu baada ya sikukuu, wakiwa na wazazi wao wanieleze shida ni nini"  Alisema Kolombo.


Hali hiyo imedhihilishwa na takwimu za mtihani wa kidato cha pili ambayo imeonyesha idadi ya watoto waliosajiliwa kufanya mitihani ni 2813, waliofanya mtihani ni 2593 na ambao hawakufanya mitihani ni wanafunzi 220 kutokana na sababu mbalimbali.


Hayo yamejiri tarehe 21.12.2023 kwenye kikao cha tathmini ya Elimu kidato cha pili kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti baada ya kundi kubwa la wanafunzi kushindwa kufanya mitihani na wengine kufeli.


Vilevile amewaagiza walimu kuwa na ushirikiano mzuri kuanzia ngazi za chini katika muundo wa Serikali  kuhusiana na utoro na utoaji taarifa kwenye Kamati ya ulinzi na Usalama kupitia Polisi kata ili kuweza kufanya ufumbuzi wa haraka kabla mambo hayajaharibika.

Awali kabla ya Mkuu wa Wilaya kutoa maagizo hayo  Wakuu wa shule  kutoka shule mbalimbali walitoa taarifa za mwenendo wa elimu katika  shule zao ambapo walisema chanzo cha utoro mashuleni kwa kiasi kikubwa kinahujumiwa na wazazi ambao husisitiza watoto wao kutofanya vizuri wakidai hawana fedha za kuwasomesha.


Hata hivyo Walimu hao walisema vyanzo vingine vya kushindwa kufanya mitihani kwa wanafunzi hao  mashuleni vinatokana na  ujauzito kwa watoto wa kike, utoro, nidhamu mbaya kati ya wazazi walimu na wanafunzi, ajira za utotoni, vigodoro, uangalizi hafifu wa wazazi kwa watoto wao na matumizi ya bangi.

Wakitoa mapedekezo ya nini kifanyike maoni  mengi yamekuwa na mfanano kulingana na changamoto za kimazingira kufanana ambapo wamesema kuwa kuna umuhimu wa kuunda Sheria ndogo ndogo zitakazoweza kuwabana wanafunzi na watuhumiwa, wazazi wa wanafunzi kuchukuliwa hatua Kali, kukomesha ajira kwa watoto, kuvunja vijiwe na mageto mitaani n.k.


Shule ambazo baadhi ya wanafunzi hawakufanya mitihani ni Sekondari ya Mjawa, Zimbwini, Msafiri, Dimani, Mahege, Ruaruke, Mtanga Delta, Mtawanya, Nyamisati, Kikale, Mchuckwi na Mlanzi.

Akiwakilisha Wenyeviti wa Bodi za shule , Mwenyekiti wa Bodi ya shule ya Sekondari Msafiri Bw. Lazaro Lukonge amempongeza Mkuu wa Wilaya Kanali Kolombo kwa kuona umuhimu wa kuchukua hatua ili kupunguza tatizo lililopo ndani ya Wilaya. Pia amemuomba Kanali Kolombo kuwalinda Wakuu wa shule kwani wengi wao hufanya kazi kwa hofu na kushindwa kutimiza wajibu wao ipasavyo.


Kikao hicho limehusisha Kamati ya ulinzi na Usalama, Wakuu wa shule, Maafisa elimu Kata, Maafisa Elimu Sekondari (W), Wenyeviti wa Bodi za shule na Polisi kata ndani ya Wilaya.


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.