• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KIKAO CHA MWAKA CHA TATHMINI YA UTENDAJI KAZI WA IDARA YA AFYA, USTAWI WA JAMII NA LISHE WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/ 2024.

Posted on: September 6th, 2024

Idara ya Afya, Ustawi wa jamii na Lishe ya Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti imefanya kikao cha siku 2 ili kutathmini hali ya Utendaji kazi wa Idara hiyo kwa mwaka uliopita. Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Halmashauri tarehe 05 na 06 Septemba, 2024.

Akitoa neno la utangulizi mbele ya mgeni rasmi wa kikao hicho, Maganga Mkuu (W) Dkt. Dismas Masulubu amesema lengo la kikao hicho ni kufanya mapitio ya takwimu mbalimbali kwa pamoja ili kujua mahali walipotoka na walipo, kubaini changamoto na kuweka mikakati.

Lakini pia alisema kikao hicho kitawawezesha wafawidhi kubadilishana Uzoefu na kuchukua hatua za kufanya maboresho katika afua ambazo kituo hakifanyi vizuri.

“Kikao kinatoa fursa kwa CHMT na Wafawidhi kuona umuhimu wa matumizi ya ukusanyaji wa takwimu kwa ubora wake, kuziingiza kwenye mifumo rasmi na kuzichakata kwaajili ya kufanya maamuzi pamoja na kutoa fursa ya kujengeana uwezo na mbinu mbalimbali katika kuboresha huduma mahala pa kazi” Alisema Dkt. Masulubu.

Baada ya kusikia Ikama ya Watumishi katika idara hiyo kama ilivyowasilishwa na Katibu wa Afya, Makamu mwenyekititi wa Baraza la Madiwani Kibiti Mh. Omary Twanga alisema:

“Nilikuwa na maneno mengi ya kuwaambia leo kutokana na malalamiko ya Wananchi lakini kwa hiki nilichosikia na kuona leo nimeishiwa maneno yote. Kwasababu kama kituo kinatakiwa kuwa na Watumishi 10 na sisi kwetu kuna 2 au 1 lazima utoaji wa huduma uwe wa kusuasua, lakini pamoja na hayo tunawaomba sana Watumishi wetu endeleeni kuchapa kazi kwa bidii, sisi madiwani tutawaelewesha Wananchi na tunaahidi ushirikiano wa kutosha kwenu”.

Kikao hicho pia kimehudhuriwa na wadau mbalimbali wa Afya kama vile ANJITA, PASADA na THPS ambao kwa pamoja walielezea majukumu yao na namna wanavyoshirikiana na Serikali na Idara ya Afya katika utoaji wa huduma kwa Wananchi.

“Tunashukuru kwa kuona umuhimu wetu hivyo kutupa nafasi kushiriki kwenye kikao hiki, kwakuwa wadau tunatoa huduma na misaada kule kwa wananchi ni wengi tunaomba Mganga Mkuu utukusanye kwa pamoja ili kuweka mikakati tusiwe tunatoa misaada inayofanana. Kama mmoja ameleta daftari basi mwingine alete nguo hapo tutakuwa tumewasaidia sana” Alisema mwakilishi wa PASADA.

Akiongea kwa niaba ya Mgeni Rasmi Afisa Tarafa wa Kibiti Bw. Salim Mzaganya amesema ni wakati sasa Watoa huduma wa Afya kuwa na mifumo rafiki ya utoaji wa huduma inayoendana na ukuaji wa teknolojia, kwani Ulimwengu umeshahama kutoka kwenye mifumo ya Analogi na sasa tupo kwenye dunia ya kidigitali.

“Idara ya Afya ni moja ya maeneo yenye malalamiko mengi kule kwa wananchi, nawaomba sana watoa huduma jitahidini kutoa huduma  bora. Yale yote mnayofanya kule sirini sisi yanatufikia hadharani, kwahiyo kama ilivyo kauli mbiu ya kikao chenu huduma bora kwa wananchi wa Kibiti ndo ikawe kipaumbele chenu” Alisema Bw. Mzaganya.

Aidha Bw. Mzaganya alifunga kikao hicho kwa kuwaasa wataalam hao kwenda kutoa huduma kwa weledi wa hali ya juu, kutoa taarifa kwa wakati pale mtu anapojaribu kuwaingilia katika taaluma zao na mwisho kabisa kusimamia na kutunza vyema miradi inayokwenda kwenye vituo vyao.

Mwisho, Idara imetoa zawadi ya vyeti vya pongezi kwa vituo vyote vya kutolea huduma za Afya vilivyofanya vizuri katika nyanja mbalimbali ikiwemo kusimamia vizuri mapato ya vituo kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KANALI KOLOMBO AIPONGEZA MARINE PARKS KUANZISHA MIUNDOMBINU YA KUHIFADHI NA KULINDA MATUMBAWE BAHARINI

    May 10, 2025
  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.