• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

KILELE CHA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA WANAWAKE NA WATOTO

Posted on: December 10th, 2022

Halmashauri ya wilaya ya Kibiti chini ya Idara ya Maendeleo ya jamii na Taasisi mbalimbali za kisheria imehitimisha siku 16 za kupinga ukatili kwa wanawake na watoto ambayo ilianza Novemba 25 mpaka disemba 10 ulimwenguni ikiwa ni  siku ya haki za binadamu Duniani.

Akimkaribisha Mgeni rasmi Afisa maendeleo ya jamii wa wilaya Khamisi Mnubi amewapongeza wote waliojitokeza kukamilisha siku 16 za kupinga ukatili wa kinjinsia ambapo  ni kumbukizi ya mauaji ya kikatili ulimweguni kote.

Kilele cha maadhimisho hayo kimefanyika katika jengo la kupumzikia abiria katika stendi ya mabasi Wilayani humo ambapo mgeni rasmi alikuwa Diwani wa Kata ya Kibiti Mhe. Hamidu Ungando. Katika maadhimisho hayo  amesema suala la ulinzi wa watoto na wanawake ni mtambuka hivyo kila mwananchi anawajibu wa kuwalinda wanawake Pamoja na Watoto.  Pia amewataka wanawake na watoto wenyewe kuwa majasiri na kutoa taarifa  pindi wanaposikia au kushuhudia vitendo hivyo ili taratibu za kisheria zifuatwe mara moja kwa wote wanaohusika na vitendo vya ukatili kwa makundi hayo.

Akisoma taarifa ya maadhimisho hayo, Afisa maendeleo ya jamii anayesimamia watoto na wanawake Agness Willa amesema migogoro ya ndoa ni chanzo kikubwa cha ukatili wa watoto. katika wilaya ya Kibiti 2021-2022 matukio 24 ya ubakaji yaliripotiwa, watoto 62 walitelekezwa, 27 walijeruhiwa Kwa vipigo na 84 walitambuliwa wakifanya biashara katika maeneo ya stendi huo ni ukatili pia.

Vilevile Afisa ustawi wa jamii  Kata ya Kibiti Bi Hajrat Kidua  ametoa rai Kwa jamii Kwa ujumla kuwajibika kupambana na masuala mazima ya ukatili wa kijinsia kwa kuendelea kutoa elimu kwenye majukwaa mbalimbali. Pia kuijengea jamii uwezo kujua mifumo ya ulinzi na utetezi wa haki za binadamu ikiwa ni pamoja na kujua maeneo husika ya kutoa taarifa wanapokutana na changamoto hizo.

Aidha Jovita Mlima askari polisi kutoka dawati la jinsia ,yeye amewahimiza watoto na wazazi kutoa taarifa Kwa wakati kwani bila kutoa taarifa ni vigumu kutambua ukatili unaofanyika majumbani.

Naye Mwenyekiti wa Kata ya Kibiti, ameeleza kuwa unyimwaji wa chakula ni sehemu ya ukatili pia, amewataka wazazi na jamii kwa ujumla kulima mazao ya muda mfupi na kujiandikisha kupata mbolea mapema ili waweze kulima na kupata mazao ya kutosha, jambo litakalosaidia kupunguza utumikishwaji wa watoto (vibarua).

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.