• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

MAADHIMISHO YA UPANDAJI MITI KIMKOA YAFANYIKA KIBITI.

Posted on: April 10th, 2024

Siku ya upandaji miti kitaifa huadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe 1 Aprili, Kampeni hii ilianza mwaka 1999 ikiwa na lengo la kutoa hamasa kwa wananchi kupanda miti  na kuiendeleza misitu. Maaadhimisho ya siku hii Kimkoa na Kiwilaya hutegemea na kiwango cha unyevu kilichopo katika ardhi kufuatia na mvua. Hivyo kwa Mkoa wa Pwani mwaka huu 2024 maadhimisho haya yamefanyika jana tarehe 09 Aprili 2024 kwa kupanda miti katika Shule ya msingi Kibiti iliyopo Wilayani Kibiti.

Akisoma risala kwa mgeni rasmi Afisa misitu mkoa wa Pwani Bw. Pierre Protas amesema Mkoa wa Pwani ulifanikiwa kupanda miti 8,876,640 kwa mwaka 2022/2023 na inatarajia kupanda jumla ya miche 10,436,494 kwa msimu huu wa mwaka 2023/2024 ambayo imezalishwa na inaendelea kupandwa katika maeneo mbalimbali.

Akimuwakilisha mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amesema anawashukuru sana wananchi wote wa Kibiti na Mkoa wa Pwani kwaujumla kwa kujitokeza kushiriki zoezi hili la kuupanda miti katika eneo la shule ya msingi Kibiti.

“Zoezi hili la upandaji miti mashuleni ni endelevu na linaunga mkono Kampeni ya ‘SOMA NA MTI’ iliyozinduliwa Januari, 2022 kwa lengo la kuhamasisha wanafunzi juu ya umuhimu wa kupanda miti” Alisema Kanali Kolombo.

Vilevile Kanali Kolombo alisema  zoezi hili ni muhimu sana ili kupunguza kutokea kwa athari za mabadiliko ya tabia ya nchi kama vile ongezeko la joto, mvua zisizotabirika na za uhakika pamoja na vimbunga.

“Upandaji miti na utunzaji wa mazingira ni suluhu pekee yenye uhakika wa kutunusuru na majanga haya, ndiyo maana tunasisitiza upandaji miti na kauli ya mwenge wa uhuru mwaka huu 2024 inahimiza hivyo kwa kusema ‘Tunza mazingira shiriki uchaguzi wa serikali za mitaa kwa ujenzi wa taifa endelevu ‘” Alisema Kolombo.

Akihitimisha hafla hiyo kanali Kolombo amewataka Viongozi wa Wilaya, Halmashauri na TFS kuhakikisha misitu iliyohifadhiwa inatunzwa vizuri ikiwa ni pamoja na kuzuia shughuli yeyote ya kibinadamu ndani ya misitu kama vile uchomaji wa mkaa, uvamizi wa mifugo, uchimbaji wa mchanga, kokoto, kilimo na makazi kwenye misitu mambo yanayochangia uharibifu wa misitu kwa kiwango kikubwa.

Jumla ya miti 1030 (1000 ya mbao na 30 ya matunda) imepandwa jana kataika maadhimisho haya.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.