• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

MAONYESHO YA BIASHARA MKOA WA PWANI KUWA YA KITAIFA IFIKAPO 2025.

Posted on: December 18th, 2024

Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Selemani Jafo, ameagiza maonyesho ya biashara na uwekezaji ya Mkoa wa Pwani kuwa ya kitaifa kuanzia mwaka 2025, yakisimamiwa rasmi na Wizara ya Viwanda na Biashara.

Dk. Jafo alitoa agizo hilo leo disemba 17.2024, wakati akizindua maonyesho ya biashara yanayofanyika kwa mara ya nne mkoani humo, yakihusisha wawekezaji na wajasiriamali wadogo kutoka mkoa huo. Waziri huyo alisema kuwa maonyesho ya Mkoa wa Pwani yamekuwa yakifikia viwango vya kitaifa, na hivyo ni muhimu kuyaendeleza kwa ngazi hiyo ili kuvutia wawekezaji zaidi.

“Kuanzia mwaka 2025, maonyesho haya yawe ya kitaifa na yasimamiwe na Wizara ya Viwanda na Biashara kama yalivyo maonyesho mengine makubwa nchini. Hili ni agizo rasmi kwa Katibu Mkuu wa Wizara,” alisema Dk. Jafo.


Aidha, Waziri Jafo alizitaka taasisi wezeshi kuhakikisha haziwi kikwazo kwa wawekezaji wanaotaka kuwekeza nchini, akisisitiza umuhimu wa utoaji wa huduma bora ili kuvutia wawekezaji wapya.

Katika hatua nyingine, alihimiza wazalishaji wa bidhaa kuhakikisha wanazingatia ubora wa bidhaa zao ili ziweze kushindana kwenye masoko ya ndani na kimataifa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, alitoa wito kwa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kuhakikisha wanajenga bomba la gesi katika maeneo ya uwekezaji mkoani humo ili kurahisisha upatikanaji wa nishati ya gesi kwa viwanda.

Kunenge alisema maboresho makubwa kwenye sekta ya umeme yameongeza uzalishaji wa megawati kwa asilimia 19, hatua ambayo imerahisisha uzalishaji kwa wawekezaji wa viwanda. Hata hivyo, alisema baadhi ya wawekezaji wanahitaji nishati ya gesi kwa ajili ya uzalishaji.

Mkoa wa Pwani kwa sasa una viwanda 1,533, kati ya hivyo viwanda vikubwa ni 78. Mkoa huo pia unaendelea kuboresha miundombinu ya uwekezaji, huku maeneo makubwa zaidi yakitengwa kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda vipya.


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.