• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

MWENGE WA UHURU 2023 WARIDHIA JUMLA YA MIRADI 15 YA MAENDELEO KIBITI.

Posted on: May 21st, 2023

.

21.5.2023

Mwenge wa uhuru 2023 umeridhia miradi 15 ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti yenye jumla ya sh.Bil 1.3 kwa kuikagua, kuzindua, kufungua sambamba na uwekaji wa mawe ya msingi baada ya kujiridhisha na kutoa maelekezo mbalimbali kwa kuchagizwa na Kauli mbiu yenye usemi usemao Tunza Mazingira Okoa Vyanzo vya Maji, kwa Ustawi wa Viumbe hai kwa Uchumi wa Taifa.

 "Tumepokea taarifa ya miradi, tumekagua na kuridhishwa na miradi yote pamoja na nyaraka zote", Alisema Kaim.

Hayo yamebainishwa na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Taifa 2023 Ndg. Abdallah Shaib Kaim baada ya Mwenge wa Uhuru kumulika na kuridhia miradi hiyo.

Mkimbiza Mwenge Taifa Ndg. Abdallah Shaib Kaim ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti kwa kusimamia vizuri miradi ya Maendeleo inayotekelezwa kwa fedha za Serikali na mapato ya ndani huku akimshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyotoa fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya Maendeleo Wilayani Kibiti na Nchi nzima Kwa ujumla.

"Nichukue fursa hii kuwapongeza Viongozi wote wa kibiti kutokana na utendaji wenu na itoshe kusema kwamba, Mwenge wa Uhuru, unatambua mchango wenu mkubwa katika kupigania maendeleo ya Wilaya hii." Alisema Abdallah Shaib Kaim.

Aidha Kaim ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti kutafuta vyanzo vipya vya mapato ambavyo vitasaidia kuongeza ukuaji wa pato la wilaya na kuendelea kujiletea maendeleo.

Akikagua mradi wa ujenzi wa nyumba ya wageni Top 5 amewataka wakazi wa kibiti kujifunza kupitia Mwekezaji huyo alimaarufu kwa jina la mjomba Dani  kuwekeza ndani ya Wilaya jambo linaloonyesha Uzalendo Mkubwa na litakalosaidia kukuza pato la wilaya.

Akisoma Salam za Mwenge wa Uhuru  ndg. Kaim amewataka wananchi kuhakikisha wanahifadhi mazingira hususani katika vyanzo vya maji ili kuweza kuendana na mabadiliko ya tabia nchi ambayo yamekuwa ni tatizo kubwa Duniani kote.


Hata hivyo katika salamu hizo za Mwenge ndg Kaim amesisitiza wananchi kuhakikisha wanapambana na adui wa Maendeleo (Rushwa) kwa kuepuka kushiriki aina yoyote ya rushwa na Kwa kutoa taarifa za viashiria vya rushwa na ushahidi mahakamani ili kufanikiwa kudhibiti changamoto hiyo. Licha ya Salamu hizo pia amewataka wananchi kukabiliana na mapambano dhidi ya madawa ya kulevya kwa kuepuka kujishughulisha na uuzaji na uzalishaji wa dawa hizo Pamoja kuendelea kuwaelimisha walioathiriwa na dawa hizo kutorudia tena kutumia dawa hizo.

Hakuishia hapo katika salamu za Mwenge amewasihi wananchi kupambana na mapambano dhidi ya Malaria yenye kauli MBIU isemayo, "zero malaria inaanza na Mimi, chukua hatua kuitokomeza"

Bila kusahau ulaji wa lishe bora yaani mlo kamili, kwani lishe Bora hujenga afya imara na kuleta maendeleo ya afya imara kwa watu wote, hususani katika makundi 5 ya vyakula ambayo ni ulaji wa mbogamboga kwa wingi, mafuta, nafaka kidogo, matunda na sukari.

 Mbali ya salamu hizo vilevile amewasisitiza wananchi wa kibiti kukabiliana na mapambano ya ugonjwa wa Ukimwi kwa kuimarisha USAWA, kutokomeza ukatili wa kijinsia, kuhudhuria vituo vya afya kupima afya na kuanza kutumia dawa za kufubaza endapo mtu atagundulika ameathirika

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.