• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

NMB WATOA MADAWATI 120 KWA SHULE ZA MSINGI 5 KIBITI.

Posted on: August 30th, 2024

Jana Agosti 29, 2024 Benki ya NMB imekabidhi Madawati 120 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kibiti ikiwa ni sehemu ya kurudisha shukrani kwa Jamii ya Kibiti kwa kuendelea kuiamini na kutumia benki hiyo. Msaada huo ni matokeo ya Ombi la Mh. Mkuu wa Wilaya Kibiti Kanali Joseph Kolombo alilotoa mapema mwezi Januari mwaka huu katika kikao chake na Wadau wa Elimu.

Kanali Kolombo aliwaomba Wadau hao kusaidia miundo mbinu katika Sekta ya Elimu hususani Meza na Viti kwa Shule za Sekondari pamoja na Madawati kwa Shule za Msingi, kwani Wanafunzi wengi bado wanakaa chini. Hivyo basi NMB wamefanikisha Jambo hilo kwa kuchangia madawati 120 yenye thamani ya Sh. Milioni 12.

Akikabidhi Madawati hayo Meneja wa NMB Kanda ya Dar-es-Salaam na Pwani Bw. Seka Urio amesema, NMB imefarijika sana ilipopokea maombi ya kuchangia madawati ili kuboresha mazingira ya kusomea kwa Wanafunzi na kuona imeheshimika kushiriki kuunga Mkono jitihada za Mhe. Rais katika kuboresha miundo mbinu ya Elimu nchini.

“Kibiti tuna Wateja wengi sana kama vile Walimu, Wafanyabiashara na Wananchi, hivyo kile ambacho NMB inakipata kwa kufanya biashara na jamii hiyo, baada ya kulipa kodi ya Serikali huwa tunatenga 1% ya faida na kurudisha kwa jamii tunayofanya nayo kazi huku kipaumbele chetu siku zote kikiwa ni Elimu, Afya na wale wanaopata changamoto ya Majanga. Kwahiyo madawati haya ni sehemu ya fedha hizo”. Alisema Bw. Urio

Aidha Kanali Kolombo ameishukuru sana benki hiyo kwa Madawati na misaada mingine iliyowahi kutolewa hapo awali kama vile Bati 120 zilizotolewa mwezi Januari mwaka huu ambazo zilisaidia kupaua nyumba za walimu waliokuwa hawana pa kukaa.

“Tunawashukuru sana NMB kwa misaada mingi mnayoendelea kutuletea Kibiti maana si Madawati haya tu yapo yale ya 2018 ambayo tumepita huko darasani na kuona yametunzwa vyema na bado yapo imara. Lakini pia nakumbuka mlituletea bati 120 ambazo zilisaidia kupaua nyumba za Walimu, Sasa naona ipo haja ya nyie kutenga siku 1 mje kututembelea ili muone misaada mliyotoa inaendeleaje, Sisi Kibiti tunaahidi kuitumia kama ilivyokusudiwa” Alisema Kanali Kolombo.

Akitoa salamu za chama Katibu wa CCM Wilaya ya Kibiti Ndg. Malik Magimba ameishukuru sana benki ya NMB kwa moyo wao wa ukarimu na jitihada zao za kuiunga mkono Serikali katika sekta ya Elimu huku akiwasisitiza kutokusita kuendelea kutoa misaada pale watakapoombwa tena kwani chanamoto bado ni nyingi kwa Wilaya ya Kibiti.

Naye Mwenyekiti wa Hamashauri ya Wilaya ya Kibiti Ndg. Ramadhani Mpendu kwa niaba ya baraza la Wahe. Madiwani ameishukuru sana benki hiyo kwa kuwa msaada huo waliotoa utapunguza adha ya madawati katika kata 5 kati ya 16 za Hamashauri ya Wilaya ya Kibiti.

Mwisho kabisa Halmashauri imetoa cheti cha pongezi kwa NMB kwa kutambua mchango wao katika Sekta ya Elimu.

Madawati hayo yamegawanywa katika shule 5 kama ifuatavyo: Madawati 40 Shule ya Msingi Kitundu, Madawati 25 Shule ya Msingi Jaribu Mpakani, Madawati 25 Shule ya Msingi Mkwandara, Madawati 20 Shule ya Msingi Maparoni na Madawati 10 Shule ya Msingi Kinyanya.


Wote kwa pamoja, Walimu na Wanafunzi waliopokea madawati hayo wameahidi kuyatunza vyema.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.