• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

SEMINA KWA MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA PWANI

Posted on: December 8th, 2022

Serikali ya Tanzania ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia kwa ufadhili wa Serikali ya Uingereza kupitia mfuko wa UK Aid imetoa semina kwa waandishi wa habari mkoa wa  Pwani juu  mradi kabambe wa shule bora nchini , kwa dhumuni la kuboresha elimu na kumfanya mtoto kupata msingi mzuri kuanzia ngazi za awali.

Katika mkutano huo Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Zuwena Omari amesema Serikali imeshirikisha waandishi wa habari katika mpango huo wa kuboresha Elimu kwa sababu inatambua na kuthamini mchango wao katika Elimu. Pia ametumia fursa hiyo kuwaagiza Waandishi wa Habari Mkoa wa Pwani kutumia kalamu zao vizuri katika kuandika habari za mradi wa Shule Bora ambao ni mpango mkakati wa kutoa elimu bora kwa watoto wa madarasa ya awali na msingi.

Amesema hayo alipokuwa akifungua mafunzo ya siku moja ya waandishi wa habari na maafisa habari wa mkoa wa Pwani, wenye lengo la kuinua kiwango cha elimu kwa watanzania wote, kwa kuhakikisha kuna mazingira salama ya kujifunzia kwa wanafunzi wa jinsia zote.

Vile vile Bi Zuwena ameeleza kwamba mradi wa shule bora nchini una malengo mannne, la kwanza ni KUJIFUNZA (kuhakikisha watoto wanajifunza shuleni), la pili KUFUNDISHA (mfuko wa msaada wa UKAID utaunga mkono na kuimarisha kazi ya ufundishaji Tanzania), la tatu JUMUISHI (kuhakikisha watoto wote wa kitanzania wakiwemo wenye uhitaji maalum mashuleni wanakuwa katika Mazingira salama na rafiki ili kuwawezesha kumaliza Elimu ya msingi  na wanaendelea na Elimu ya Sekondari), na la nne KUJENGA MFUMO (mfuko wa UK Aids,utaunga mkono serikali na kuimarisha ili kupata au kuwa na thamani ya fedha katika utoaji wa Elimu katika ngazi zote Toka chini hadi Taifani).

Aidha, Zuwena amezielekeza  Halmashauri za Mkoa wa Pwani kuhakikisha zinasimamia vizuri mradi huo ili uweze kuleta mafanikio makubwa hapa nchini hususani katika kuimarisha elimu kuanzia ngazi za chini kwa kusudi la kuwajengea msingi imara mpaka wanamaliza Elimu ya Sekondari.

Kwa upande wa Afisa Elimu Mkoa wa Pwani Sara Mlaki amesema kwamba kwa kipindi cha mwaka mmoja mradi wa Shule bora umekua na mafanikio makubwa changamoto nyingi zinazowakatisha masomo wanafunzi hususani wakike zimepungua kama vile ndoa za utotoni, mimba katika umri mdogo utoro n.k

Awali Afisa mahusiano wa mradi huo, Raymond Kanyambo, alifafanua  kuwa Shule bora ni mradi wa Serikali unaolenga kuinua kiwango cha elimu katika ngazi ya awali na msingi nchini ambapo jumla ya  Mikoa tisa nchini ukiwemo Mkoa wa Pwani, kigoma,Dodoma, Tanga, Mara, singida,Rukwa, simiyu na katavi zitanufaika.

Mpaka Mradi unakamilika utagharimu  bajeti ya Paundi za kiingereza milioni 89 sawa TSh bilioni 271 ambapo program ikienda vizuri pia kuna uwekekano ukawa endelevu Kwa miaka mitatu tena endapo utafanya vizuri.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.