• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

SERIKALI YAWASHIKA MKONO WAHANGA WA MAFURIKO KIBITI

Posted on: April 8th, 2024

7.4.2024

Ofisi ya Waziri Mkuu kitengo cha maafa imetoa msaada kwa wahanga waliofikwa na Mafuriko yaliyoharibu mali mbalimbali kutokana na  mvua zinazoendelea nchini katika baadhi ya Kata  za wilaya ya Kibiti hususani mazao.

Akikabidhi msaada huo  kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Kamishna msaidizi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Sera, Bunge na Uratibu Ndg. Khamis Lutengo amesema baada ya kupokea taarifa na kutokana na hali halisi ilivyo wameona ni vema kuwapa mkono wa pole wakazi wa Kibiti ili kuweza kuokoa maisha ya watu waliothirika na Mafuriko hayo.

"Waziri Mkuu yuko pamoja nanyi wakazi wa Kibiti, ameona ni vema kuwashika mkono wa pole kuweza kuokoa watu waliathirika na Mafuriko haya" Alisema Kamishna huyo.

Msaada uliotolewa ni mahindi Tani 20, ndoo za maji 300 zenye ujazo wa lita 10, mablanketi 510, neti za mbu 540 mahema makubwa mawili, na Moja kwa Moja msaada huo utapelekwa  katika Kata zote 5 ambazo wananchi wameathiriwa na Mafuriko.

Licha ya kupokea msaada huo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Ndg. Rashid Mchatta amesema ngazi ya Mkoa inakwenda kuitisha kikao cha wadau kuona namna ya kuendelea kutoa michango na misaada mingine kadri itakavyowezekana ili kuweza kuwasaidia wananchi hivyo, ameiagiza kamati ya maafa (W) ya Kibiti kuweka kumbukumbu ya taarifa sahihi katika akaunti  ya makusanyo pamoja na kuimarisha ulinzi wa msaada uliopokelewa ili ukafikie wahanga waliofikwa na madhira hayo ipasavyo.

Kwa upande wa Wilaya ya Kibiti Katibu Tawala wa Wilaya Bi. Maria Katemana akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ameishukuru Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia kitengo cha maafa kwa kujali na kuona umuhimu  wa kutoa msaada huo kwa wahanga wa Mafuriko, hasa katika kipindi hiki chenye uhitaji  sana. Pia Bi Katemana ameahidi kuwa  watahakikisha  wanasimamia vizuri zoezi la usambazaji wa msaada huo, ili iweze kuwafikia walengwa waliokusudiwa.

Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Ndg. Hemed Magaro amesema kamati ya maafa ngazi ya Wilaya imejipanga vizuri kuhakikisha wanawafikia walengwa wote katika Kata zote 5 za Mtunda, Msala, Maparoni, Kiongoroni na Mbuchi zilizokumbwa na Mafuriko kwa wakati huu.

Naye Diwani wa Kata ya Mtawanya Mhe. Malela Tokha baada ya kushuhudia mapokezi ya msaada huo, amemshukuru Mhe. Rais Dkt. SSH kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu na kudai kwamba anaamini  msaada huo unakwenda kuwasaidia wananchi  waliopatwa na maafa na kuwa faraja kwao katika kipindi hiki kigumu wanachopitia.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.