• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

SERIKALI YAWEKA WAZI MWENENDO WAKE WA KUTATUA NA KUSIKILIZA CHANGAMOTO ZA WALIMU. WALIMU KUPANDA MADARAJA KWA MSEREREKO NA KAWAIDA.

Posted on: June 3rd, 2024

01.06.2024

Afisa Elimu Mkoa wa Mbeya Mwl. Kiduma Mageni kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu OR-TAMISEMI Dkt.Charles Msonde amewasilisha ujumbe Serikali  namna inavyosikiliza na kutatua changamoto za Walimu nchini.

Ujumbe huu unakuja ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais kwa OR-Tamisemi kuhakikisha wanasikiliza na kutatua changamoto za walimu nchi nzima.

Akiwa Wilayani Kibiti Mwl. Mageni amesema katika utekelezaji wa agizo hilo  tathmini iliyofanyika imebaini changamoto kubwa za Walimu ni upandaji wa madaraja, mabadiliko ya vyeo vya muundo baada ya kujiendeleza kielimu, malipo ya arrears, likizo na uwepo wa lugha zisizo na staha wanapofuatilia stahiki zao.

Kwa upande wa upandaji wa Madaraja nchini Mageni amesema  zaidi ya Walimu 54,000 watarajie watapandishwa madaraja kwa mserereko na wengine 52,000 kupandishwa kawaida.


Hata hivyo Mageni amesema Tamisemi imeagiza kuhakikisha kuwa katika Mazingira ya kazi kunakuwa na nidhamu, haki, mshikamano  na uwazi hususani katika malipo ya likizo, (DEO/MEK) kuidhinisha likizo mapema na kusimamia uwepo wa mpango wa uendaji likizo wa watumishi (Leave roster) kuanzia ngazi ya shule kwa kuwa na orodha kamili kabla ya kupelekwa utumishi.

Mbali na hayo Mageni amewasihi walimu kuendelea kuchapa kazi kwa bidii wakati Serikali ikiendelea kutatua changamoto zao huku ikitarajia mabadiliko makubwa  kupitia maboresho yanayofanyika.

Mara baada ya kupokea ujumbe huo Katibu Tawala wa Wilaya ya Kibiti Bi.Maria Katemana amesema ngazi ya Wilaya wameyapokea maelekezo yote na  watahakikisha wanatekekeza kama walivyoelekezwa.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Ndg. Hemed Magaro amesema kupitia ujumbe huo Serikali itegemee kupata mabadiliko makubwa kutoka Wilaya ya Kibiti katika Idara ya Elimu.

Mwisho baadhi ya Walimu kwa niaba ya Walimu wote wamemshukuru Mjumbe huyo kwa ujumbe aliowafikishia wakisema Walimu wamepata Ari na nguvu mpya ya utendaji na kwamba wako imara wakiwa na utayari mkubwa wa kubadilika.


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.