• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

SHIRIKA LA NORWAY, KKKT DAYOSISI YA MASHARIKI NA PWANI, WAADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA KIBITI.

Posted on: June 17th, 2024

15.6.2024.

Ilipokuwa imesalia siku moja kuelekea maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika, Shirika la msaada la Norway wakishirikiana na KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani waliadhimisha siku hiyo katika Kata ya Bungu Wilaya ya Kibiti kwa lengo ya kuwakumbuka watoto wa Kitongoji cha Soweto nchini Afika Kusini ambao waliouawa tarehe 16.6.1976 kutokana na ubaguzi wa rangi.

Akitoa utambulisho Mratibu wa maadhimisho kutoka Shirika hilo la kidini Bi. Latifa Agustino amewasihi wazazi/walezi/jamii kuyafanya maadhimisho hayo kuwa maalum kwa ajili ya kuzungumzia changamoto na mahitaji ya watoto wa kiafrika kwa kutafakari na kuhakikisha watoto wanaishi katika mazingira salama.

Kaulimbiu ya mwaka 2024 inayosema “Elimu jumuishi kwa watoto izingatie maarifa maadili na stadi za kazi” ilinogeshwa zaidi na maigizo, shairi na ngonjera zenye jumbe mbalimbali kwa jamii kupitia maadhimisho hayo .

"Kaulimbiu hii imetoa wito kwa wazazi Serikali, Walezi na Wadau kutimiza wajibu katika kuimarisha mifumo ya ulinzi na makuzi ya mtoto ili aweze kukabiliana na changamoto ya ongezeko la vitendo vya ukatili ili aweze kupata haki bila ubaguzi." Alisema Agatha.

Bi Agatha Lema ambaye ni Afisa Miradi aliendelea kusema kuwa maadhimisho hayo ni fursa ya kufanya tathmini ya utekelezaji wa sera za kitaifa zinazohusu maendeleo ya watoto kwa kuwapatia stahiki zao kama vile Elimu, Afya, Maadili bora , Ulinzi pamoja na kukemea vitendo viovu wanavyofanyiwa watoto kama vile kubakwa, kulawitiwa, Vipigo, Matusi, Kutelekezwa n.k

Vile vile  Afisa Miradi huyo amewataka wazazi kuwapatia watoto maarifa, kuwafundisha maadili mema, uadilifu, sambamba na kuwafundisha kufanya kazi mbalimbali bila kusahau kuwapa watoto fursa ya kusikilizwa haswa wanapoelezea changamoto zao.

Aidha Bi. Johnmary Richard akimwakilisha Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Kibiti amewataka wazazi na jamii kujitafakari kwa kina na kuchukua hatua madhubuti kutimiza wajibu wao kwa kuwalea watoto ipasavyo.

Naye Afisa Elimu Maalum Sekondari Wilaya ya Kibiti Mwl. Loisa Lambileki amewataka wazazi kutenga muda wa kuwa karibu na watoto ili kuweza kuwasikiliza na kubaini changamoto walizonazo sambamba na mahitaji yao.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KANALI KOLOMBO AIPONGEZA MARINE PARKS KUANZISHA MIUNDOMBINU YA KUHIFADHI NA KULINDA MATUMBAWE BAHARINI

    May 10, 2025
  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.