• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

SIKU YA MTOTO WA AFRIKA YAFANA KIBITI.

Posted on: June 16th, 2023


WAZAZI/JAMII WATAKIWA KUSIMAMIA MALEZI YA WATOTO.

Leo ni siku ya Mtoto wa Afrika, siku hii huadhimishwa barani Afrika ifikapo Juni 16 ya kila mwaka ikiwa ni utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Nchi huru za Afrika zenye dhamira ya kuwakumbuka Watoto wa kitongoji cha Soweto nchini Afrika kusini waliouawa kikatili na utawala wa ubaguzi wa rangi tarehe 16/06/1976.

Maadhimisho hayo yenye  kauli mbiu isemayo; “Zingatia usalama wa mtoto katika ulimwengu wa kidijitali” mwaka huu katika Mkoa wa Pwani kimkoa yameadhimishwa wilayani Kibiti Kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ya maendeleo kama vile PASSADA, CAMFED, JICHO ANGAVU, INTERFAITH, HUDUMA YA WATOTO NA VIJANA KKKT n.k.

Katika maadhimisho hayo Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa  Pwani Mhe. Abubakar Kunenge ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo amesema, jukumu la malezi ya watoto ni la wazazi na jamii kwa ujumla.

"Wazazi au walezi chunguzeni watoto wenu kabla na baada ya kutoka shule, ili kujua mazingira ya watoto, " Alisema Kanali Kolombo.

Kutokana na vitendo vya ukatili vinavyojiripotiwa, Kanali Kolombo amewataka wazazi kuacha tabia ya kumaliza changamoto hizo kijamii/kifamilia na badala yake kutoa taarifa mapema ili hatua stahiki zichukuliwe huku akitoa namba za kupiga bure kuripoti vitendo hivyo vinapotokea.

Katika maadhimisho hayo Afisa maendeleo ya jamii Mkoa wa Bi Grace Tete amesema kuwa wazazi wamekuwa chanzo kikubwa cha watoto kuharibikiwa, kwa kutojali kufuatilia mwenendo na makuzi ya watoto hususani katika matumizi ya simu katika umri mdogo.

Akisoma risala ya watoto kwa niaba ya watoto wenzake, Lilian Luhinda mwanafunzi shule ya msingi Kingwira amesema, Halmashauri ya wilaya Kibiti kupitia idara ya maendeleo ya Jamii, imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha ulinzi na usalama wa mtoto unaimarika, ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa klabu za watoto mashuleni, masanduku ya maoni, utoaji wa vifaa vya shule kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi, utoaji wa elimu ya ukatili dhidi ya watoto mashuleni, elimu ya lishe, na huduma za matibabu kwa wahanga wa ukatili.

Vilevile mtoto Lilian alisema, pamoja na jitihada zilizofanywa na Serikali bado kuna changamoto kubwa zinazowakabili watoto katika wilaya ya Kibiti, kwa asilimia kubwa  Wazazi/ walezi wameoneka kuwa chanzo cha changamoto hizo kwa kushindwa kutoa huduma za msingi zinazohitajika kwa watoto (chakula, mavazi, malazi, elimu na mwongozo, huduma ya afya, kinga)  na kusababisha watoto kushiriki katika shughuli hatarishi kwa ajili ya kujitafutia mahitaji.

Hata hivyo Lilian aliendelea kusema kuwa kukosekana kwa malezi sahihi kutoka kwa wazazi au walezi imekuwa sababu ya watoto wengi kukosa mwelekeo mzuri wa maisha na kujiingiza katika makundi hatarishi ambayo husababisha watoto kukabiliwa na matukio ya ukatili kama (ubakaji, vipigo, ajira kwa watoto, utelekezwaji, mimba za utotoni ) mambo yanayosababisha watoto kushindwa kutimiza ndoto zao.

Aidha kutokana na changamoto wanazopitia,watoto wameiomba serikali kuwachukulia hatua kali kisheria watu wote wanaofanya ukatili dhidi ya watoto ili iwe fundisho kwa watu wote. Pia wameiomba serikali kuendelea kutoa elimu ya ukatili na lishe mara kwa mara kwa wazazi na walezi katika shule za sekondari na msingi hasa katika shule ambazo zipo Delta au katika kata ambazo matukio mengi ya ukatili yameripotiwa (Kibiti, Bungu, Mjawa na Salale).

Licha ya ombi hilo pia watoto wameiomba Serikali kuwaelekeza  Wazazi na walezi kufanya wajibu wao kikamilifu katika kuwalea watoto na kuwahudumia watoto wao huku wakiisihi Serikali kuendelea kuweka mazingira rafiki katika shule ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa chakula au uji ili kuwawezesha watoto kuwa na hali nzuri wakati wa masomo.

Afisa maendeleo ya jamii Mary Sanga Akisoma taarifa ya Wilaya ya kibiti kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji amesema katika Wilaya wamefanikiwa kuwajengea uwezo wazazi/walezi pamoja na Watoa huduma mbalimbali kwa watu wapatao 250 kwa kuwapa elimu ya Malezi na makuzi ya watoto wao. Vile vile Mary alisema, wamepokea mashauri mbalimbali  yapatayo 508 ya ukatili  wa kingono, ukatili wa kimwili, n.k.

"Katika kuhakikisha usalama wa watoto mpaka sasa mashauri 111 yamefikishwa katika vyombo vya dola (Polisi, Mahakamani) na watoto 315 wamepatiwa vifaa vya shule,  huduma za afya, Elimu ya ukatili na ushauri nasihi" Alisema Mary.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.