• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

TAASIS YA ELIMU TANZANIA KUANZA UFUATILIAJI WA UTEKELEZAJI WA MATUMIZI YA MWALIMU MSAIDIZI JAMII WA ELIMU YA AWALI KATIKA VITUO VYA UTAYARI

Posted on: December 22nd, 2022

Taasisi  ya Elimu Tanzania (TET)  imeanza zoezi la ufuatiliaji  wa utekelezaji wa matumizi ya mwalimu msaidizi jamii wa elimu ya awali katika vituo vya utayari vyenye kusudi la kumuandaa mtoto  ambaye hajawahi kupata elimu ya awali, kuwa na utayari wa kuanza Darasa la Kwanza mwaka 2023.

Ufuatiliaji huo umelenga kuona jinsi  mwalimu anavyoweza kutumia  vitabu vya hadithi vinavyowezesha  mtoto kuanza darasa la Kwanza na uhalisia ukaonekana Kwa jinsi watoto walivyohadithia hadithi mbalimbali,utambuzi wa namba ,Picha na uimbaji wa nyimbo Kwa umahiri.

Akiwa Wilayani Kibiti Mwesiga Kabigumila  ambaye ni Mratibu wa Proramu ya shule Bora Kutoka Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) amesema vituo hivyo vimeanzishwa chini ya program ya  Shule Bora kwa lengo la  kuwapunguzia safari watoto wenye umri mdogo, wasitembee umbali mrefu kuitafuta elimu lakini kumuandaa mtoto kuwa tayari kuanza shule.

Hata hivyo Mratibu Kabigumila  ameridhishwa na namna Walimu Wasaidizi  Jamii wa walivyotumia zana, njia na mbinu mbalimbali za kuwaaanda watoto kuwa tayari kuanza shule, katika ziara hiyo  watoto wameonesha uchangamfu na utayari wa kuanza darasa la kwanza Kwa vitendo kutokana na uelewa walioupata darasani.


Vilevile Kabigumila ambaye pia kitaaluma ni Mwalimu amewapongeza Walimu  Wasaidizi wa Jamii kwa kukubali jukumu la kuwaandaa watoto hao katika vituo vyote vya mkoa wa Pwani  hususani Kibiti,pia amewapongeza wazazi wote waliokubali watoto wao kuandaliwa katika vituo hivyo huku akiwasisitiza kuhakikisha wanapata eneo la kujenga vyumba vya madarasa ya kusomea.wakati huo huo amewataka wazazi wote kuwaandikisha watoto  katika shule mama huku wakiendelea kusoma walipo chini ya uangalizi wa shule mama wakati shule shikizi zikiandaliwa kujengwa .


Awali kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kibiti Mwalimu Violet Mahimbo ambaye ni Afisa Taaluma Msingi,mbele ya Mratibu aliomba watoto waendelee  kufundishwa kwa ajiri ya utayari wakati Uongozi wa Wilaya na wakazi wa maeneo husika wanapambana kuhakikisha eneo la ujenzi wa madarasa linapatikana .

Pia  mwalimu Mahimbo amefurahishwa kwa uchangamfu ambapo watoto wameonyesha utayari wa kuanza darasa la kwanza huku akisisitiza wazazi kuandikisha watoto wenye utayari kuanza darasa la kwanza na awali Kwa ambao hawajapata utayari huku akitoa pongezi kwa Walimu Jamii (MJM) wa shule shikizi Pombwe Kuu, King’ongo na Uchembe kwa kazi nzuri inayoonekana kwani watoto wameonesha wapo tayari kuanza shule.

Kwa nyakati tofauti waheshimiwa madiwani, wenyeviti wa Vijijina Vitongoji wameshukuru program ya Shule Bora na Taasisi ya Elimu Tanzania Kwa kuanzisha mradi na kufuatilia kwa umakini, kwani uanzishwaji wa Madarasa ya utayari yamesaidia wazazi kufanya shughuli mbalimbali za  uzalishaji Mali Kwa uhuru uwepo wa kituo cha utayari karibu unawapunguzia safari za kupeleka watoto shule na kuwafuata wakati wa kurudi majumbani.pia wameahidi kushirikiana na serikali pamoja na wananchi kuhakikisha vyumba vya Madarasa vinapatikana Katika maeneo ya karibu.

Kwa upande wake mwakilishi wa  wananchi wa Pombwe Kuu ameomba Jengo la shule shikizi lifanyiwe maboresho huku akisema suala la eneo la Ujenzi wa shule wawaachie litapatikana.wakati huo huo wananchi wa kitongoji Cha King’ongo na kata ya Mjawa waneomba ngazi ya Taifa  kuendelea kuwasemea ili kuisaidia upatikanaji wa maendeleo ya Elimu nchini hususani maeneo ya vijijini.

Zoezi la ufuatiliaji limeongozwa na Viongozi wa TET nchini, Wilaya ya Kibiti limefanyika katika kata ya Mjawa kituo cha utayari Uchembe na Kata ya Kiongoroni katika Kijiji cha Pombwe kuu na kitongoji cha King’ongo .

Shule bora ni mradi wa  Serikali unaofadhiliwa na serikali ya Uingereza kupitia mfuko wake wa misaada UKAaid unaolenga kuinua kiwango cha elimu katika ngazi ya  Elimu ya awali na msingi nchini ambapo jumla ya  Mikoa tisa nchini ukiwemo Mkoa wa Pwani, kigoma,Dodoma, Tanga, Mara, singida,Rukwa, simiyu na katavi zitanufaika na mradi huo.

Katika ziara hiyo ya siku mbili Mratibu wa Programu ya Shule Bora Kutoka TET,  iliambatana na Afisa Elimu Maalum wa Wilaya wa wanafunzi wenye uhitaji Maalum Shabani Makuka,yeye ametoa wito kwa jamii kuwafichua na kutowaficha watoto wenye ulemavu kwani Serikali inawatambua na kuwathamini kwa kuhakikisha wanapata Elimu kama wengine.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.