• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

TaTEDOSESO KUANZISHA MASHAMBA YA MITI ILI KURAHISISHA UPATIKANAJI WA MALIGHAFI ZA KUZALISHA MKAA.

Posted on: July 24th, 2024

22.07.2024

Shirika lisilo la kiserikali la TaTEDOSESO limetoa mafunzo muhimu ya utunzaji wa mazingira na uchomaji wa mkaa endelevu katika Kijiji cha Ngulakula na baadae wataendelea katika vijiji vingine Wilayani Kibiti.

Akitoa mafunzo hayo Mwezeshaji Shima Sago kutoka TaTEDOSESO amesema ili kuwa na uchomaji wa mkaa endelevu, wameanzisha utaratibu wa mashamba ya miti  kwa ajili ya kupata malighafi ya kuchoma mkaa.

Mradi huo utasaaidia wachoma mkaa, wajasiriamali na wakulima wa kawaida kuanzisha mashamba ya miti ambapo watapewa miche bure pamoja na mafunzo ya kuyasimamia.

Katika Mafunzo hayo washiriki wamefundishwa uvunaji endelevu wa miti unaohusisha uchaguaji wa miti ya kuvuna (selective harvest), uvunaji wa kupumzisha maeneo, na matumizi ya Matanuru ya kisasa.

Vilevile Mratibu wa Mradi huo Afisa Maliasili Ndg. Dotto Mandago amesema mradi huo utasaaidia kuhifadhi misitu kwa wanajamii wa vijiji 10, na kupandisha mnyororo wa thamani kwenye uchakataji wa mazao ya misitu.

Akizungumzia Sheria na kanuni za misitu Afisa maliasili Ndg. Swalehe Kilindo amesema watatoa mwongozo  wa njia bora za uchomaji wa mkaa kwa kutumia matanuru ya kisasa kama ambavyo Gn no. 417 kifingu cha 10 inavyoekekeza.

Nae Afisa nyuki kutoka wakala wa misitu Tanzania (TFS)-Kibiti Bi Paschalina Mwenesi amesema, katika kuhakikisha mradi unakuwa endelevu, watasimamia na kusaidia kwa karibu zaidi vikundi vya wafugaji wa nyuki vitakavyoanzishwa na TaTEDOSESO, sambamba na kusimamia rasilimali za misitu kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

Aidha washiriki wa mafunzo hayo wameishukuru TaTEDOSESO kwa kuleta mafunzo hayo na wamesema  wamejifunza vitu vingi ambavyo walikuwa hawavijui na zaidi wamepewa mbinu mpya ya utengenezaji wa tanuru la kisasa la kuchomea mkaa  tofauti na walivyozoea.

Licha ya shukrani hizo washiriki hao wamesema Kupitia uanzishwaji wa mashamba ya miti ya kuzalisha malighafi ya kuzalisha mkaa watapata fursa ya kuongeza kipato kwani wapo watakaokuja kununua miti hiyo mashambani hivyo, watafanya biashara ya kuuza miti.

TaTEDOSESO limeendesha mafunzo hayo chini ya udhamini wa Umoja wa Ulaya kupitia Wizara ya Fedha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Lengo kubwa katika mradi huu ni kuimarisha utunzaji wa mazingira kwa kuacha kukata miti hovyo kwa kusimamia  uchomaji wa mkaa kwa kutumia malighafi chache na kupata mkaa mwingi kwa matanuru ya kisasa n.k.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.