• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

TOTAL ENERGIES WAKABIDHI MADAWATI 130 KWA SHULE YA MSINGI JARIBU MPAKANI NA SHULE YA MSINGI KITUNDU WILAYANI KIBITI.

Posted on: September 24th, 2024

24.09.2924

Katika kusheherekea  miaka 100 tangu kuanzishwa kwa Kampuni ya mafuta ya Total Energies Duniani kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Leo septemba 24 wamekabidhi jumla ya madawati 130 katika Shule ya Msingi Jaribu mpakani na Shule ya Msingi Kitundu zilizopo Wilayani Kibiti  ikiwa ni sehemu ya kurudisha shukrani kwenye jamii.

"Kwa hapa Tanzania Kampuni hii ilianzishwa mwaka 1969 na katika maadhimisho haya ya miaka 100 tumeona ni vema faida tuliyotengeneza tuilete Kibiti," Alisema Mpangile.


Akikabidhi madawati hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Sheria na Mahusiano kutoka Total Energies Bi. Getrude Mpangile amesema madawati 65 yatakwenda Kitundu na mengine 65 yatakwenda jaribu Mpakani. Pia akatumia fursa hiyo kuwasisitiza Wanafunzi wa shule hizo kusoma kwa bidii na kupandisha ufaulu ili waweze kufanya vizuri katika mitihani yao na kuendelea na masomo ya Sekondari mpaka elimu ya juu.

Vilevile Mpangile ameipongeza Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa kuwa na miongozo mizuri waliojiwekea ya kutambua changamoto mashuleni na zinapotokea fursa kuelekeza penye uhitaji kama ambavyo wamewaelekeza TOTAL kupeleka msaada Kibiti.

Hata hivyo Bi Mpangile amesema licha ya kurudisha shukrani Kupitia Sekta ya elimu, kwa Total Energies Sekta hiyo ni kipaumbele hivyo wataendelea kusaidia kwa 90% kwani ni imani yao kupitia elimu watazalisha wasomi wengi kwenye vizazi vijavyo.


Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa TEA Bi.  Mwanahamis Chambega ametoa Rai kwa walimu, wanafunzi na Wazazi kuhakikisha wanatunza vizuri madawati hayo ili yakadumu na kuendelea kusaidia wanafunzi wengine kwa miaka mingi zaidi.

Katika mapokezi hayo Afisa Elimu Divisheni ya Awali na Msingi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Mwl. Zakayo Mlenduka amewashukuru Total Energies kwa kuupa umuhimu uhitaji wa Kibiti bila kusahau TEA kwa kuusemea uhitaji huo kwa wadau hao wa maendeleo.

Aidha akipokea msaada huo Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo ameseishukuru Kampuni ya Total Energies kwa msaada waliotoa kwani unakwenda kupunguza changamoto iliyopo ya upungufu wa madawati huku akipongeza Mamlaka ya elimu Tanzania kwa kuwatafikia wafadhili hao.


"Kibiti tuna upungufu wa madawati 2767, kwa mapokezi ya madawati 130 uhitaji unaendelea kupungua ahsanteni sana, msisite kuja tena mtakapoguswa” Alisema Kolombo.


Nae Diwani wa Kata ya Mjawa Mhe. Ramadhani Chepa akatoa shukrani za Kata hiyo huku akiwapongeza TEA kwa kuwa msaada mkubwa lakini pia akawasisitiza Total Energies kuendelea kuwashika mkono kwani bado wanauhitaji mkubwa kwa upande wa madawati na hata kwa ujenzi pamoja na ukarabati wa shule hiyo ambayo ni kongwe.

Kwa nyakati tofauti Walimu Wakuu wa Shule hizo pamoja na wanafunzi wametoa shukrani zao za dhati kwa wafadhili hao wakiwaomba kutosita kwa kipindi kingine endapo watahitajika kwani msaada huo unakwenda kuwa chachu ya elimu licha ya changamoto zilizopo kama vile utoro, ufaulu, uchakavu wa majengo n.k

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.