• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

UVCCM KIBITI WAANZA ZIARA YA KUTEMBELEA KATA KWA KATA.

Posted on: September 4th, 2023


Mwenyekiti wa Jumuiya ya umoja wa Vijana Wilaya ya Kibiti (UVCCM) Amina Mkomboya leo tarehe 4.9 2023 ameanza ziara ya siku 11 ya kutembelea Kata za Wilaya ya kibiti kujionea shughuli zinazoendelea, changamoto zilizopo na kuona namna ya kuzitatua.

Akiwa katika Kata ya Bungu Bi Amina, amezindua tawi la kijiwe cha makao makuu ya UVCCM Kata ya Bungu A ambapo amesema amefarijika sana kushiriki katika tukio hilo muhimu.

Vilevile Bi Amina amewatembelea wanafunzi wa darasa la Saba shule ya msingi Bungu A na kutoa zawadi ya kalamu boksi 8 huku akiwasisitiza wanafunzi hao kuwa watulivu, kuzingatia waliyofundishwa na kufanya vizuri mitihani yao ya mwisho inayotarajiwa kufanyika septemba 13 na 14 mwaka huu.

"Tunatarajia mtafanya vizuri mitihani yenu na matokeo yenu kuwa mazuri someni kwa bidii " Alisema Amina.

Hata hivyo Mwenyekiti Amina amewashukuru wananchi wa Bungu kwa kumwamini na kumchagua, yuko tayari kuwatumikia muda na wakati wowote.

" Ahsanteni sana kwa kuniamini, niko tayari kuwatumikia, kuwapigania, na kuwasemea changamoto zenu zote, karibuni milango ya ofisi yangu iko wazi". Alisema Amina.

Katika ziara hiyo Katibu wa Jumuiya ya umoja wa vijana (UVCCM) Bw. Angelo Madale amewataka wanauvccm kuhuisha chama kwa kuzingatia maelekezo waliyopewa kwenye matawi ya ofisi zao, kwani uhai wa Chama ni pamoja na kufanya vikao, ziara ,kulipa ada na kuwa na kadi.

Hata hivyo amewapongeza Viongozi wa chama na Serikali ( Rais, Mbunge, na Diwani ) kwa namna wanavyohakikisha maendeleo yanapatikana Kata ya Bungu na Wilaya ya Kibiti Kwa ujumla.

Aidha ameagiza vijana kujitokeza kwa wingi kuomba nafasi za chipkizi zilizotangazwa ili waweze kushiriki na wenye sifa kuweza kugombea nafasi hizo.

Pia Katibu Madale amewataka wazazi na walezi wote kufuatilia mienendo ya watoto wao, wanapocheza, wanapoenda shule na kurudi ili kuimarisha maadili ambayo yamekuwa ni changamoto kubwa katika ulimwengu wa sasa na kuwasisitiza kusoma kwa bidii kwani elimu ndiyo urithi wa maisha yao.

Nao Wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji Wilaya ya Kibiti Bw.Athman Mtoliya na Bi. Shamsa Mkulugo wamewataka wananchi na UVCCM kuendelea kuwaunga mkono Viongozi wao ili kuendelea kupata maendeleo mbalimbali yanayotekelezwa katika Wilaya ya Kibiti hususani Kata ya Bungu.

Akifunga kikao hicho, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Kata ya Bungu Said Omary amesema ujio wa UVCCM Kata ya Bungu ni faraja kubwa huku akielekeza Jumuiya hiyo kuwa imara, kuzingatia yaliyozungumzwa na kuyatekeleza kwa vitendo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.