• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

UZINDUZI WA KAMATI YA UHAMASISHAJI NA UELIMISHAJI WA MAGONJWA YA MLIPUKO.

Posted on: February 17th, 2023


Tahere 17/02/2023 Wizara ya Afya chini ya ufadhili wa shirika la Afya Duniani (WHO) wamefanya uzinduzi wa kamati za uhamasishaji na uelimishaji  juu ya magonjwa ya Mlipuko katika Ukumbi wa mikutano uliopo katika  Jengo la Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.

Katika uzinduzi huo  Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo, ameitaka jamii kuchukua tahadhari za kukabiliana na magonjwa ya Mlipuko ikiwemo Cvid 19, Kipindupindu, Ebola, Kimeta na mengineyo kutokana na hatari kubwa ya kusababisha vifo.

Pia, ameipongeza Serikali chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada kubwa wanazozifanya za kukabiliana na magonjwa hayo hatari katika jamii.

Kanari Kolombo alisema magonjwa ya mlipuko yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara katika jamii, ambapo kwa Tanzania yalianza miaka mingi iliyopita hivyo kuna umuhimu wa kupata elimu kuyadhibiti kabla hayajatokea.

Pia aliipongeza na kuishukuru Serikali kupitia Wizara ya Afya inavyofanya jitihada za kudhibiti magonjwa hayo na kusema wataendelea kuunga mkono kwa kutoa elimu kwa wananchi wa Kibiti.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kibiti Mohamed I. Mavura, alisema kuwa jamii ya Tanzania imepitia katika changamoto ya magonjwa mbalimbali ikiwemo Uviko 19, hivyo kuna umuhimu mkubwa wa kukabiliana na magonjwa ya mlipuko kwani yana athiri afya ya jamii na uchumi.

“Kwa kuwa Kibiti sio kisiwa, hatuna budi kujifunza mbinu na namna mbalimbali za kujikinga , kuwakinga na wengine Pamoja na kukabiliana na changamoto za mlipuko zinapojitokeza kwani mlipuko wa magonjwa unapojitokeza mahali kuna athari nyingi zikiwemo za kiuchumi”

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Kibiti Elizabeth Oming’o, alisema wamejipanga vyema kutekeleza kampeni hiyo ya kuelimisha jamii kukabiliana na magonjwa hayo ya mlipuko

"Tunapongeza Wizara ya Afya kwa kuja na mpango wa kutumia kamati ambayo inahusisha makundi mbalimbali hivyo wataisimamia vyema kupitia mipango yao," alisema Oming’o.


Kwa upande wake Mratibu wa Elimu ya Afya kwa umma kutoka Wizara ya Afya Dr. Johnson Mndeme alisema kwa awamu wa kwanza uzinduzi wa kamati hizi utafanyika kwa mikoa minne ambayo ni Tanga, Pwani, Geita na Manyara ambapo wanaendelea kuifikia mikoa mingine mikoa mingine.

Vilevile amesema Wizara ya Afya ikishirikiana na Shirika la Afya Duniani imeanzisha kamati za kutoa Elimu juu ya magonjwa ya milipuko kwa jamii, na kamati hizi zinazoundwa na wajumbe 45 zitakuwa katika ngazi zote kuanzia kata, wilaya Hadi mkoa. Aidha Wizara imefikia uamuzi huu baada ya kuona Serikali inatumia rasilimali fedha nyingi sana kupambana na magonjwa ya mlipuko yanapojitokeza hivyo ni vema jamii ikawa na desturi ya kupata Elimu kuliko kusubiri janga litokee.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.