• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

“WAFANYAKAZI ENDELEENI KUFANYA KAZI KWA BIDII” – RC KUNENGE

Posted on: May 2nd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge amewataka Wafanyakazi wa Mkoa huo kufanya kazi kwa bidii ili kuongeza tija katika utendaji kazi na kuboresha maslahi yao wenyewe, kwani tija ikiwepo kutakuwa na ziada kubwa ambayo inaweza kufanya maboresho zaidi.


"Endeleeni kufanya kazi kwa bidii kwa sababu siku zote maslahi Bora hupatikana pakiwa na tija" Alisema.

Mhe. Kunenge amesema hayo alipokuwa katika maadhimisho ya sikukuu ya Mei Mosi ambayo Kimkoa yamefanyika katika Wilaya ya Kibiti yakiwa na Kauli mbiu isemayo Nyongeza ya mishahara ni Msingi wa mafao Bora na Kinga dhidi ya hali ngumu ya maisha.

Akizungumzia changamoto mbalimbali zilizoziwasilishwa kupitia risala ya Wafanyakazi Mkuu huyo wa mkoa wa Pwani amewasihi Wafanyakazi kuendelea kuwa wavumilivu wakati wakisubiri matamko ya Viongozi wa Kitaifa kwani kuna masuala mengine ni ya kisera na tayari Serikali imekwishaanza kuyashughulikia ikiwa ni pamoja na suala la kikokotoo cha wastaafu, n.k

Hata hivyo amesema kuwa katika kukabiliana na changamoto zolizopo Mheshimiwa Rais anahangaika sana kuangalia namna gani anaongeza uwezo wa serikali kuboresha mazingira ya kazi nchini kama vile kuboresha mazingira ya shule ambazo watoto wanasoma, sekta ya afya na tayari ameahidi kuboresha makazi ya Wafanyakazi katika sekta ya elimu na afya na yote haya hufanyika kulingana na bajeti inayokuwepo.

Aidha kwa mazuri hayo amewataka Wafanyakazi kuzungumzia kazi nzuri anazofanya Rais Dkt Samia katika kuhudumia Wananchi nchini "mnapopata nafasi semeni mazuri yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ambaye anawapenda na kuwajali Wafanyakazi nchini kwani anawahakikishia usalama na haki za Wafanyakazi kazini"

Mwisho Mkuu huyo wa Mkoa amemwagiza Katibu Tawala wa Mkoa  Ndg. Rashid Mchatta kuhakikisha anachukua hatua kwa Taasisi au watu binafsi wanaokiuka maelekezo ya Serikali katika utendaji wa kazi.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph kolombo ameomba Serikali kuangalia namna ya kusaidia usafiri wa uhakika kwa Walimu wanaofundisha katika Shule za maeneo ya Kata za Delta ambako kutoka sehemu Moja kwenda nyingine hutumia mitumbwi au boti

Mbali na hayo pia katika maadhimisho hayo kumefanyika harambee ya kuchangia fedha mbalimbali kwaajili ya kupeleka misaada kwa Waathirika wa mafuriko wilayani Rufiji na Kibiti ambapo zaidi ya sh. milioni 4,400,000/- zilipatikana kwa ahadi na feda taslimu kwa  ujumla.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.