• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

WAFUGAJI WOTE AMBAO MIFUGO YAO HUHARIBU MAZAO YA WAKULIMA KATIKA KIJIJI CHA MUYUYU KUKAMATWA

Posted on: December 29th, 2022

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Meja Edward Gowele ameagiza kukamatwa kwa wafugaji wote ambao mifugo yao huharibu mazao ya wakulima katika Kijiji cha Muyuyu Kata ya Mtunda ili Sheria iweza kufuata mkondo wake.

Meja Gowele amemuagiza Mkuu wa Polisi (OCD) Wilaya SSP H.F. Ramadhani kukamata mifugo yote inayozagaa mtaani na kuharibu mazao ya watu sambamba na kuwakamata wafugaji wa wanaoachia mifugo yao na kusababisha migogoro. Pia OCD ameagizwa kusimamia kikamilifu endapo ikitokea tena suala la udhalilishwaji wa wanawake huku akisisitiza waotendewa kutoa taarifa bila uwoga ikiwa ni pamoja na kutoa ushahidi mahakamani.

Hata hivyo amesema katika mikutano iliyopita alitoa maelekezo kwa wafugaji kujiandikisha ili wapewe maeneo yao (RANCHI) na kuyaendeleza huku akisisitiza kila upande kufuata taratibu na Sheria zilizopo kwa kuhakikisha eneo la kilimo kinafanyika kilimo na eneo la ufugaji ni malisho ya mifugo.

“Waliolima eneo la wafugaji acheni mara moja vivyo hivyo wanaofuga na kulisha eneo la wakulima hameni”alisema Gowele

Amebainisha hayo alipokuwa akijibu malalamiko ya wakulima ambayo yamekuwa yakijirudia mara kwa mara katika Kata hiyo ambayo ni kiungo kwa uzalishaji wa zao la ufuta na uchangiaji wa Mapato katika  wilaya ya kibiti

Vilevile Katika kutatua kero hizo amemuagiza Mkurugenzi Mavura kuwa na mthamini wa mazao Wilayani ambaye atakuwa anatoa thamani ya uharibifu kwa ajili ya fidia.Pia amemuagiza Mwenyekiti wa Kijiji Hassan Mtwendwe kusimamia uundwaji mpya wa Kamati ya usuluhishi ambayo hutakiwa kuwa katika kila Kijiji ikiwa na wajumbe kutoka kwa wakulima na wafugaji kwa maelekezo ya kanuni na taratibu za kamati hiyo.

Kwa upande wa changamoto ya  eneo la kilimo mwekezaji wa kilimo cha Mpunga Kata ya Mtunda Khamis kambagwa ameridhia agizo la Serikali,hivyo wakulima wajiandae kupata mbegu za kupanda kwani yeye atasafisha na kulima hekari 180 ndani ya siku 12.Pia ameomba kupewa heka moja kati ya 180 ambazo atalima ikiwa ni sehemu ya  shamba darasa ambapo atatumia fursa hiyo kuwafundisha kilimo cha kisasa kinachosaidia kupata mazao mengi katika eneo dogo.

Aidha Mhe.Mkuu wa Wilaya amesema suala la changamoto ya mawasiliano ya mitandao ya simu amelibeba,kwa upande wa barabara upembuzi yakinifu umekwishafanyika huku akisisitiza kuwa upatikanaji wa haki mahakamani hutegemea na utayari wa ushahidi jambo ambalo ni changamoto kwa wakazi wengi wa maeneo hayo na hukusu mipaka shauri hilo linajadiliwa katika ngazi za juu Idara ya ardhi hivyo kuwe na subira wakati mgogoro huo unachakatwa.

Awali Diwani wa kata ya Mtunda Omary Twanga ,ameishukuru kamati ya ulinzi na usalama iliyoambatana na Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi pamoja na Wataalam wa ardhi kwa kuhudhuria mkutano huo wenye faraja kuhusu malalamiko ya wakulima wakisigana na wafugaji.pia amewataka wakazi wa Kijiji cha Muyuyu kuendelea kuwa wavumilivu na kuepuka kuchukua Sheria mkononi kwani malalamiko yao yanafanyiwa kazi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa barabara .



Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KANALI KOLOMBO:SERIKALI INATAMBUA MCHANGO WA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI

    June 12, 2025
  • PPRA KANDA YA PWANI YATOA MAFUNZO KUHUSU SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA NA MFUMO WA KIELEKTRONIKI WA UNUNUZI WA UMMA

    June 12, 2025
  • KANALI KOLOMBO AIPONGEZA MARINE PARKS KUANZISHA MIUNDOMBINU YA KUHIFADHI NA KULINDA MATUMBAWE BAHARINI

    May 10, 2025
  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.