• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

WAKAZI WA KIBITI WAHAMASIKA KULIMA PAMBA

Posted on: March 22nd, 2024

19.3.2024

Ikiwa ni sehemu ya utekelezaji, Bodi ya Pamba Tanzania, Kampuni ya Pamba ya Rufiji (Rufiji cotton limited) kwa kushirikiana na Idara ya kilimo ya Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti imefanya zoezi la uhamasishaji wa kilimo cha pamba katika vijiji 12 vya  Kata 8 za wilaya ya Kibiti ambapo wameonekana kuhamasika.

Wakitoa taarifa ya zoezi hilo maafisa ugani wamesema, jumla wakulima 659  wamejisajili tayari kwa kuanza kilimo na kuchukua mbegu ambayo imekwisha sambazwa katika Kata 11 na mpaka sasa Tani 15 za mbegu ya pamba zimekwishapokelewa ambapo zinatarajiwa kupandwa katika hekari 1500 katika vijiji vyote.

Hayo yamejiri katika kikao kazi cha ufuatiliaji tathmini ya maendeleo ya kilimo cha pamba zoezi lililofanyika katika vijiji mbalimbali vya Wilaya ya Kibiti ambapo maafisa ugani wametoa taarifa na kuja na maazimio mkakati kuweza kuimarisha kilimo hicho.

Hivyo katika kikao hicho wameazimia kila Afisa ngazi ya Kata, vijiji na vitongoji kuendelea kutoa elimu juu ya kilimo cha pamba,  pembejeo kufikishwa mapema kwa  wakulima na kuitumia kama ilivyoelekezwa kama viua wadudu na bomba zenye ubora. Maafisa ugani kuwezeshwa mafuta ili kuweza kuwafikia wakulima ,kuanzisha mashamba ya mfano pia kuwe na ufuatiliaji angalau kila mwezi kuhakikisha kilimo hicho kinafanyika ipasavyo Wilayani Kibiti n.k

Hata hivyo Meneja wa Bodi ya Pamba Kanda ya mashariki Ndg. Emmanuel Mwangulumba amesema licha ya kusambaza viuatilifu na mabomba  watatoa maboza mawili, moja kwa Taasisi ya JKT Mkupuka na lingine kwa Gereza la Wilaya Mng'aru ili kuweza kurahisisha kilimo hicho.

Akizungumza kwa niaba ya Mwekezaji Bw. Lameck Mapalala amesema Kampuni ya Pamba Rufiji limited imedhamiria kushirikiana na wakulima kufufua kilimo cha Pamba Wilaya ya Kibiti, wanachohitaji ni kupewa takwimu za wakulima waliojisajili, kuna jumla ya hekari ngapi zitakazolimwa kila Kijiji  ili waanze kazi haraka bila kupoteza muda.

Naye Balozi wa Pamba Tanzania Ndg. Agrey Mwanri amemsihi Mkuu wa Wilaya kusimamia kwa nguvu zote kurejesha kilimo cha zao la pamba Wilayani Kibiti kwani, wanatarajia kwa kila Kijiji kuzalisha Tani 210,000 baada ya kilimo kuanza rasmi.

Kuhusu masoko, Balozi wa Pamba Wilaya ya Kibiti na Diwani wa Kata ya Maparoni Mhe. Bakari Mpate amewaondoa hofu maafisa ugani akisisitiza kuzalisha pamba kwa wingi kwani masoko yapo na pamba ya Kibiti inatakiwa sokoni kulingana na ubora wake.

Aidha baada ya kupokea taarifa Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo amewataka maafisa ugani wote kuhakikisha kiwango cha uzalishaji wa zao la pamba kinaendana na wingi wa mapokezi ya mbezu zilizopokelewa, huku akiahidi kuwa atahakikisha kilimo cha zao hilo kinaimarika na kuleta tija zaidi.

"Tumepokea Tani 15 za mbegu ya pamba ni nyingi, maafisa ugani mkasimamie vizuri kilimo hiki mazao yaendane na wingi wa mbegu tuliyoipokea," Alisema Kanali Kolombo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.