• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

WALIMU KATA ZA BUNGU MLANZI NA MJAWA WAPATA MAFUNZO YA KKK.

Posted on: March 1st, 2023

Kaimu Afisa Elimu divisheni ya Elimu ya awali na msingi Wilaya ya Kibiti Mwl. Costansia Assey amefungua mafunzo ya siku moja ya  KKK kwa kanda ya Bungu, inayojumuisha kata za Bungu, Mlanzi na Mjawa yaliyofanyika katika shule ya msingi Songas yenye Lengo la kutoa maarifa ya uundaji wa zana na kuandaa mazingira mazuri ya ufundishaji kwa watoto.

Mafunzo hayo ni matokeo ya mafunzo kwa baadhi ya Walimu wawakilishi yaliyoandaliwa na Mradi wa Shule Bora unaofadhiliwa na shirika la UKAID kwa lengo la kuiunga mkono Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuinua kiwango cha Elimu jumuishi pamoja na kuweka mazingira  salama ya  kujifunzia kwa wanafunzi wote wakike kwa wa kiume katika shule za Serikali ya Tanzania.


Assey ambaye ni Mwalimu wa Elimu ya watu wazima na mlezi wa Elimu  kata ya Bungu, amewataka walimu wote walioshiriki mafunzo hayo kuyapokea na kuyatumia kwa weledi ili yakalete mabadiliko kwa watoto pindi wafundishwapo darasani.

“Mafunzo haya ni ya msingi sana, husaidia kujenga uelewa wa jinsi ya kuwafundisha watoto ili wajue kusoma, kuhesabu na kuandika kwa haraka hivyo, pokeeni kwa moyo, na mafunzo haya yakawe chachu katika ufundishaji wenu. Na mara tuu baada ya mafunzo haya Idara ya Elimu inatarajia kuona tunapata mabadiliko chanya kwa upande wa KKK ”. Alisema Assey.

Katika kufikia malengo ya Watoto wote kujua KKK shuleni, nendeni mkawe na utaratibu wa kukutana na kubadilishana uzoefu wa zana na mbinu za kufundishia ili kuhakikisha watoto wanajua kusoma, kuandika na kuhesabu (KKK).Walimu wenzenu wamepewa mafunzo na baada ya kuelewa wamewafikishia maarifa waliyopata kwa kuwafundisha ili   wote mkaelewe mbinu mbalimbali za ufundishaji na ujifunzaji.


Pia kutokana na vitendo vya ukatili kukithiri mashuleni na majumbani hususani vitendo vya ulawiti, Mwl Assey amewaagiza Walimu kuwa karibu na watoto ili kuweza kutambua na kujua mabadiliko yao kwa haraka kwani vitendo hivi vinarudisha nyuma maendeleo ya Watoto kitaaluma.


Vilevile Mwezeshaji wa mafunzo hayo Mwl Regina mbilinyi  amesema mafunzo ya KKK yatasaidia kutokomeza tatizo la kutokujua kusoma ,kuandika na kuhesabu, pia kuongeza mbinu za ufundishaji na ujifunzaji na kuongeza ujuzi kwa walimu.

Mbilinyi amesema ili watoto wajue KKK wamejipanga kufundisha kwa bidii kwa kutumia zana mbalimbali walizojifunza, kutokomeza utoro na kuhakikisha watoto wanapenda shule na kufurahia masomo.

Aidha mafunzo yamehusisha Walimu Wakuu, Walimu wa Taaluma , Walimu wa darasa la awali, la kwanza, la pili na waratibu Elimu kata(MEK) ambao hawakupata bahati ya kudhudhuria mafunzo hayo chini ya mpango wa Shule Bora.



Naye mratibu wa elimu Kata ya Bungu Mohamed Mtuliakwako amewataka Walimu kutumia mafunzo hayo kuwa fursa kwa kujituma ili kuweza kupata mabadiliko ya haraka kwa watoto kwa kufanya kazi kwa bidii sambamba na uandaaji wa zana za ufundishaji.

“Tumejifunza tumeelewa, ndani ya miezi 3 tutafanya tathmini tujipime kama tumefika malengo” 


Alisema Mtuliakwako huku akimwomba Afisa Elimu kupitia mafunzo hayo kuanzishwe mashindano ya kanda katika Wilaya ya Kibiti ili kuwe na hamasa ya ufundishaji na kuweza kufuta tatizo la Watoto kutokujua KKK.


Akizungumza kwa niaba ya Walimu walioshiriki mafunzo mwl. Kisa Anyagile Mwakobela   wa shule ya msingi Pagae amewashukuru wawezeshaji kwa somo zuri kwani wamejifunza kuwa Mwalimu anatakiwa kutumia mbinu mbalimbali kufundisha, madarasa kuwa na Kona za ujifunzaji (zana) zitakazosaidia watoto kujenga uelewa wa kujifunza. Pia wamejifunza kuwapima watoto kwa kuzingatia mambo muhimu ili kutambua uelewa wa mtoto kabla na baada ya kumfundisha.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.