• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

WALIMU WA HISABATI KIBITI NDANI YA MAFUNZO YA MTAALA MPYA.

Posted on: December 8th, 2023

Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na programu ya shule bora Tanzania, imeanza kutoa mafunzo endelevu  kwa walimu kazini (MEWAKA) kwa lengo la kusimamia utekelezaji wa moduli ya HISABATI iliyoboreshwa, kulingana na rasimu ya Mtaala mpya wa Elimu ya Msingi Wilayani Kibiti.

Shule bora ni mradi wa Serikali unaofadhiliwa na Serikali ya Uingereza kupitia mfuko wa UKAID unaolenga kuinua kiwango cha elimu ya Awali na Msingi nchini. Program ya Shule Bora inatekelezwa katika Mikoa Tisa Tanzania Bara kwa  kwa Usimamizi wa Elimu ya Cambridge.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti, ambaye ndiye mgeni rasmi aliyefungua mafunzo hayo, Bw. Hemed Magaro amewataka washiriki wa mafunzo ya HISABATI kusikiliza kwa makini ili waweze kuelewa wanayofundishwa kwani baada ya kupatiwa mafunzo hayo watatakiwa kwenda kufundisha wenzao ambao hawakupata nafasi ya kushiriki.

"Ninaamini kupitia mafunzo haya mtajengeka sana na kuimarika kiufundishaji mtakaporudi kwenye Kata zenu" Alisema Magaro.

Vilevile Bw. Magaro ameishukuru shule bora kwa namna walivyofikiria na kuwapatia mafunzo hayo kwakuwa kazi ambayo haina mafunzo UFANISI wake hudorora.

"Nikiri tu kwamba, kazi ambayo haina mafunzo UFANISI wake hupungua na kusababisha kudorora kwa mbinu za ufundishaji." Alisema Magaro.

Licha ya hayo Mkurugenzi Magaro alisema Serikali imetoa fedha nyingi sana kwenye Idara ya elimu na Afya, hivyo kada ya elimu walimu mna kazi ya kuhakikisha elimu inakuwa Bora na kiwango cha ufaulu kinaongezeka maradufu.

Mafunzo hayo yatakayoendeshwa kwa siku tatu yamehusisha walimu 16 wanaofundisha somo la HISABATI, Afisa anayeshughulikia programu ya shule bora Wilaya na Afisa Elimu Divisheni ya Awali na Msingi wa Wilaya.

Lengo la mafunzo haya ni kuimarisha umahiriwa walimu na viongozi wa  Elimu  katika kutumia mbinu shirikishi za ufundishaji na ujifunzaji wa somo la Hisabati ili kuleta matokeo chanya kwa wanafunzi wote.

Aidha baada ya mafunzo haya Walimu wa hisabati wanatarajiwa kuwa na uwezo wa kuchanganua dhana mbalimbali za kihisabati, kufundisha kwa ufanisi na umahiri kwa kutumia mbinu za ufundishaji, kumudu stadi za upimaji endelevu ili kuboresha ufundishaji  na kujenga stadi za utekelezaji wa MEWAKA katika ngazi ya shule.

Katika mafunzo hayo washiriki waliwezeshwa mada mbalimbali zikiwemo:

Kutambua umuhimu wa MEWAKA na Fursa zake katika kuboresha ufundishaji na ujifunzaji.

Kutambua Changamoto katika Ufundishaji na Ujifunzaji wa Hisabati.

Kubainisha uhusiano wa kimaudhui katika ya moduli ya MEWAKA na muhutasari wa somo la Hisabati kuanzia darasa la 5-7.

Kushirikishana uzoefu kuhusu ufundishaji na ujifunzaji wa Hisabati.

Kubainisha uhusiano wa kimaudhui katika ya moduli ya MEWAKA na muhutasari wa somo la Hisabati kuanzia darasa la 5-7.

Kutumia mbinu shirikishi za kufundishia na kujifunzia somo la Hisabati.

Kutumia zana za kufundishia na kujifunzia kwa mfano Jometri, Vipimo na Aljebra.

Kubainisha uhusiano wa kimaudhui katika ya moduli ya MEWAKA na muhutasari wa somo la Hisabati kuanzia darasa la 5-7.

Kwa habari picha ni matukio ya mafunzo ya Jana tarehe 7 Disemba yanayotarajiwa kuhitimishwa tarehe 9 Disemba 2023 katika ukumbi wa shule ya wavulama Kibiti.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.