• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

WANAJAMII WA DELTA WAWEZESHWA MAFUNZO YA MNYORORO WA BIASHARA ILI WAINGIE KATIKA USHINDANI KIMASOKO.

Posted on: June 18th, 2024

12.06.2024

Shirika Uhifadhi wa ardhi oevu la Wetlands International limewezesha na kuendesha mafunzo ya kuongeza thamani kwenye bidhaa zinazotengenezwa na wajasiriamali wa maeneo ya delta  Wilayani Kibiti.

Jumla ya wanajamii 20 wa vikundi vya ufugaji wa nyuki wamepatiwa mafunzo hayo wakiwemo viongozi (Afisa Maendeleo ya jamii wa Kata na Mtendaji wa Kata) kutoka katika vijiji vya Nyamisati, Kiomboni, Mfisini, Mchinga, Jaja na Ruma.

Mafunzo waliyopatiwa yamelenga kuongeza thamani kwenye bidhaa ili wajasiriamali hao waweze kuongeza kipato zaidi na kuweza kuzalisha bidhaa ambazo zitakuwa na ushindani katika soko la ndani na nje ya kibiti chini ya Mkufunzi Frank Bisheshara kutoka SIDO, ambayo ni elimu ya mnyororo wa thamani ambapo wamefundishwa kuongeza thamani ili kupata manufaa zaidi na namna ya kuendeleza biashara.

Pia wamefundishwa  kuchakata asali,kutengeneza batiki ,upatikanaji wa masoko, namna ya kusikiliza wateja na kutoaji wa huduma kwa kutumia lugha nzuri yenye ukweli na uwazi chini ya Mkufunzi Chacha kutoka chuo cha ufugaji wa nyuki Tabora.


Katika mafunzo hayo Msimamizi wa mradi wa Wetlands international Ndg. Napoleon Frank amebainisha kuwa ni matumaini yao  baada ya mafunzo washiriki wataweza kuzalisha zaidi bidhaa mbalimbali katika maeneo wanayotoka.

Licha ya hayo Ndg Frank amesema kazi kubwa ya Wetlands International ni kuhakikisha walengwa wanachangamkia fursa wanazotoa kwani zikitumika vizuri zitapunguza utegemezi na kuwaonyesha njia mbalimbali za kujikwamua na kuongeza mnyororo wa thamani kwenye bidhaa zao watakapokuwa wakizalisha.


"Tunaamini wakufunzi kutoka Sido na chuo cha nyuki Tabora wametoa mafunzo na mbinu sahihi zitakazoweza kuwasaidia wajasiriamali hawa kuongeza thamani" Alisema Frank.

Awali akifungua mafunzo hayo Mkuu wa kitengo cha Maendeleo ya jamii Wilaya ya Kibiti Ndg. Khamis mnubi amewataka wanajamii hao kutumia vizuri fursa hiyo iliyotolewa na wetlands international kwani wao ndiyo wanufaika wakubwa hivyo wanapaswa kusikiliza vizuri ili waweze kutoka na kitu kitakachowasaidia.


" Baada ya nyinyi kupatiwa mafunzo haya leo natarajia kukuta mabadiliko makubwa kupitia vikundi vyenu” alisema Bw. Mnubi.

Zaidi ya yote Mnubi amelipongeza Shirika la Wetland International kwa namna linavyokuwa karibu na jamii husika kwa kuwezesha mafunzo mbalimbali yenye tija.


Aidha kwa niaba ya washiriki wote wa mafunzo Bi. Salma Mwinga amesema kupitia mafunzo hayo na mengine mengi yatakayokuja wanaliahidi shirika hilo kuwa hawataliangusha watawawakilisha vyema kwa kutekeleza mafunzo kwa vitendo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.