• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

WASHINDI NYERERE SUPER CUP WAKABIDHIWA ZAWADI.

Posted on: October 23rd, 2023

WASHINDI NYERERE SUPER CUP WAKABIDHIWA ZAWADI.

23/10/2023.

Mkuu wa wilaya ya kibiti Kanali Joseph Kolombo amekabidhi zawadi za washindi na wadau wa Mashindano ya NYERERE SUPER CUP 2023 leo oktoba 23, ambayo yalizinduliwa septemba 24 na kutamatika oktoba 12 katika uwanja wa Samora kwa kushirikisha jumla ya timu 6 za  KIBITI FC, BUNGU FC, MTAWANYA FC, MCHUKWI FC, DIMANI FC na JARIBU FC.

Akikabidhi zawadi hizo Mgeni rasmi Kanali Kolombo amewataka washindi wote kutumia mipira waliyopewa kwa kucheza na kujiimarisha kimazoezi  tayari kwa mechi yoyote itakayokuja kucheza nao kwa wakati wote.

"Tunataka michezo iimarike mitaani, mashuleni, vijana wapo, sasa mipira hii mkaifanyie kazi mcheze" Alisema Kanali Kolombo.

Katika makabidhiano hayo mshindi wa kwanza kutoka Kibiti FC amejipatia mipira 3  na jezi pisi mbili na mshindi wa pili ni Mtawanya FC.

Vilevile wadau wa maendeleo ya michezo waliopewa zawadi ya  jezi pisi moja moja ni Ofisi ya  Mkurugenzi Kibiti, Chama cha walimu,  Chama cha corefa kusini, Chuo cha walimu Vikindu na jezi za Marefa kutoka Kibiti Sekondari.

Hata hivyo Kanali Kolombo amekabidhi zawadi za mpira mmoja mmoja kwa shule ya sekondari Zimbwini, Ofisi ya Mganga Mkuu (W) Ofisi ya Chama cha Mapinduzi (W ), Kikosi cha 830 JKT, Ofisi ya Mkuu wa Polisi Kibiti ( OCD), Ofisi ya Maliasili, Zawadi day care , Sisa  hardware na SNKD Investment.

Aidha Kanali Kolombo ameishukuru Taasisi hiyo kwa namna inavyojitoa kuifikia jamii moja kwa moja kwani ni dhana ambayo haitatoka kwenye fikra za wananchi hususani vizazi vinavyoendelea kukua.

Awali  timu zote hizo zilipatiwa Vifaa vya maandalizi jezi pisi moja moja  na mpira mmoja mmoja  kwa ajili ya maandalizi kabla ya kuanza kwa Mashindano hayo.

Kwa upande wa Katibu wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani ndugu Omary Abdull Punzi alisema kuwa malengo ya Mashindano yalikuwa kuenzi FIKRA za waasisi wetu na kutoa Elimu ya umuhimu wa Ulinzi Shirikishi na kujiepusha na matumizi mabaya ya madawa ya kulevya nchini.

Nao baadhi ya wadau waliopati wazawadi wanesema, wamefurahi sana na kupitia Mashindano hayo, watahamadisha na wadau wengine kushiriki michezo mbalimbali kwa maendeleo ya michezo Kibiti.

Mashindano hayo yamesimamiwa na Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya KIBITI sambamba na Wadau waliofanikisha upatikanaji wa zawadi ka vile NSSF, NBC BANK,WCF, TANGANYIKA ORGANIC EMPIRE na ST DAVID COLLEGE OF HEALTH SCIENCES KIMARA TEMBONI, MONICA Foundation,Sadik Mchama na Chama Cha MPIRA mkoa wa Pwani kanda ya Kusini (COREFA).

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.