• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

WETLANDS YAFANYA MKUTANO NA WADAU MBALIMBALI WILAYANI KIBITI

Posted on: November 17th, 2022

SIKU YA KWANZA

Wetland International ni Shirika lisilo la kiserikali linalo jishughulisha na kulinda na kuhifadhi maeneo oevu, limekutana na wadau wake mbalimbali wakiwemo viongozi  na wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya kibiti kujadili namna ya kuhifadhi miti ya mikoko isipotee katika ukanda wa delta ya rufiji Wilayani Kibiti.

Mkutano huo uliodumu kwa siku mbili umefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Kibiti ukiwahusisha wadau mbalimbali ikiwa ni Pamoja na wananchi wanaoishi delta ya Kiongoroni na Salale kwa lengo la kukusanya maoni Ili kutambua namna ya kuhifadhi mikoko isitoweke.

“Tuko hapa  kujadili na kuangalia jinsi gani tunaweza kushirikiana na jamii kulinda na kuhifadhi mikoko ili tuweze kunufaika na mikoko yetu”alisema Happy.

Katika Mkutano huo mtafiti mwandamizi wa misitu na uvuvi Happy Peter amesema kati ya aina 7 za mikoko zinazopatikana Duniani, aina 6 hupatikana delta ya Rufiji katika Wilaya ya Kibiti.

Pia Bi. Happy amesema katika maeneo ya ardhi oevu faida ya uwepo wa mikoko hususani katika delta ya mto Rufiji ni Pamoja na kuweza  kutengeneza mazalia ya samaki, kupunguza ukali wa mawimbi, kuzuia taka Kwenda baharini nk. Vilevile Happy amesema mbali na faida pia kuna changamoto ambazo                                                        hujitokeza katika maeneo ya ardhi oevu  kama vile mabadiliko ya tabianchi,                                                                             uchafu wa taka zilizo kithiri  mfano chupa na mifuko ya plastiki jambo ambalo hupunguza ukubwa wa eneo la mikoko.

Aidha Mtafiti na mtaalamu elekezi Dr. Emanuel Japhet amesema shughuli za kibinadamu zinachangia kuathiri zaidi kwa asilimia kubwa ukanda wa delta, akiongea kwa msisitizo Dr. Emmanuel amesema “ni bora kuhifadhi mikoko iliyopo kuliko kuanza kupanda upya kwani gharama za upandaji ni kubwa sana”. Pia akasema mikoko ya kupandwa na binadamu ni rahisi kupotea ukilinganisha na miti ya mikoko iliyoota kiasili hivyo Kuna kila sababu ya  kutunza mikoko tuliyonayo na kuhakikisha haipotei.

Nae mratibu mfawidhi wetlands Tanzania Dr. Fredric Mngube amesema, Kuna kila sababu ya kuhakikisha mikoko inalindwa na haikatwi kwani miti hiyo inaweza kupotea kwasababu ukanda wa delta kuna jamii inayoishi na kufanya shughuli  za kibinadamu. Mngube  ameitaka jamii inayoishi maeneo ya delta kuacha tabia ya kuweka Kambi au viringe katika misitu ya mikoko, ikiwa ni Pamoja na maharamia wanao tumia mashine kukata miti hiyo.

Hata hivyo Afisa kilimo Wilaya  ya Kibiti Ndg. Ismail Bainga amependekezanjia mbadala ya kusaidia jamii kuwa na shughuli za kibinadamu za kupata kipato Kwa njia nyingine na si Kwa kuharibu mikoko kama vile kupanda chikichi, korosho za muda mfupi, ufugaji wa kuku na kuanzisha uchimbaji wa mabwawa ya Samaki ili kuweza kujikwamua kiuchumi na  kuepukana na ukataji wa miti ya mikoko.

Katika Mkutano huo ulioandaliwa na shirika la Wetlands uliwahusisha viongozi wa serikali ngazi ya Wilaya, wataalam, wawakilishi wa kulima na wafugaji kutoka maeneo ya delta.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA July 03, 2023
  • RATIBA YA KAMPENI YA UCHAGUZI MDOGO WA UDIWANI WA KATA YA MAHEGE July 03, 2023
  • Taarifa kwa Umma April 12, 2023
  • Mafunzo ya UWaWa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti March 19, 2023
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA : DUMISHENI AMANI NA UTULIVU NA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    September 20, 2023
  • WAZIRI MCHENGERWA AAGIZA VIONGOZI KUWASIKILIZA WANANCHI.

    September 13, 2023
  • UVCCM KIBITI WAANZA ZIARA YA KUTEMBELEA KATA KWA KATA.

    September 04, 2023
  • UGAWAJI WA MAENEO YA RANCHI NDOGO KWA WAFUGAJI

    September 06, 2023
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.