• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

WILAYA YA KIBITI YAPATA GARI YA USIMAMIZI IDARA YA AFYA - WAZIRI MKUU MAJALIWA ASISITIZA MAGARI KUTUMIWA KWA MALENGO YALIYOKUSUDIWA.

Posted on: December 6th, 2023

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Bw. Hemed Magaro,  amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. SSH kwa kuijali Idara ya Afya ikiwepo Wilaya ya Kibiti na kuwapatia magari yanayokwenda kuongeza nguvu kazi katika kada hiyo.

Bw. Magaro amewaagiza watumishi wa Idara ya Afya kuhakikisha  kuwa gari hilo  linakuwa chachu katika kusimamia utoaji wa huduma Bora za Afya kwa wananchi wa Kibiti na usimamizi wa miradi ya Afya kwa ujumla.

Magari hayo yamekuja ikiwa ni mpango wa Serikali kuhakikisha shughuli za Idara ya Afya zinaimarika, ambapo jumla ya magari 520 kwaajili ya ufuatiliaji na tathmini yametolewa kwa Wilaya za Mikoa mbalimbali nchini.


Akimwakilisha Mhe. Rais Dkt. SSH ambaye ndiye alikuwa Mgeni rasmi katika kilele cha tamasha la Bibititi, tarehe 3 Disemba Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa amekabidhi magari 22 kwa Wilaya za Mikoa ya Dar re Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara.

Waziri Majaliwa alikabidhi magari hayo mara tu alipowasili katika uwanja wa Ujamaa Ikwiriri - Rufiji baada ya kupokea taarifa ya kutoka kwa Waziri nchi TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa, na kisha kutembelea mabanda ya maonyesho mbalimbali likiwemo banda la OR-TAMISEMI.

"Tunamshukuru Mhe. Rais kwa kutupatia magari haya, wito wangu, kila Halmashauri ikatumie magari hayo kwa malengo yaliyokusudiwa". Alisema Waziri Majaliwa.

Hata hivyo Waziri Mkuu Majaliwa amelitaka jeshi la Polisi kuwa na utaratibu wa Polisi kata kuhudumia shule na vyuo vyote katika Kata walizopo ili kuona maendeleo ya vitendo vya ukatili wa kijinsia licha ya kuwa idadi ya Polisi ni ndogo.


Pia amewaelekeza walimu wa shule za bweni kukagua na kuona kama kuna vitendo au viashiria vyovyote vya ukatili wa kijinsia na kuwasilisha taarifa haraka kwa Jeshi la Polisi.

Akihutubia maelfu ya watu waliojitikeza katika viwanja hivyo Mhe. Majaliwa amewapongeza wanarufiji na Mbunge wa Jimbo hilo kwa maandalizi mazuri huku akisisitiza kuwa maadhimisho hayo yaendane na ushupavu, uzalendo na ukombozi aliouonyesha Bibititi katika kutafuta maendeleo.

Waziri Mchengerwa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji  akitoa taarifa ya Tamasha Hilo mbele ya Waziri Mkuu amesema, katika kumuenzi Bibititi na kwa kutambua mchango wake wa Elimu, wamefanikiwa kutoa TUZO za UFANISI na UBORA wa ELIMU na kubwa zaidi likiwa ni kuweka jiwe la Msingi la ujenzi wa Barabara ya Mohoro na kupewa jina la muasisi huyo.

Vilevile amesema shughuli zingine walizofanya katika Tamasha Hilo walitembelea shule na kufanya usafi wa mazingira , kupanda miti, kugawa vitanda shule ya Sekondari ya wasichana Bibititi, kugawa mitungi ya gesi kwa mama lishe, na kufanya Tamasha la utamaduni lililoshirikisha wasanii wa muziki na vikundi mbalimbali vya ngoma.

Licha ya shughuli hizo kwa upande wa utekelezaji wa ilani ya Chama Tawala wamegawa pikipiki na baiskeli kwa viongozi wa Chama kwenye Kata na Mashina sambamba na kufanya kikao maalum katika Ofisi hizo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.