• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

ZIARA YA MHE. MBUNGE KUTEMBELEA WANANCHI WA KATA ZA VISIWANI

Posted on: November 13th, 2022

Mbunge wa Jimbo la kibiti Mhe. Twaha  Mpembenue ameanza ziara ya siku 4 katika visiwa vya  Kata ya Kiongoroni na Msala (delta) ikiwa ni sehemu ya kurudisha shukrani kwa wananchi kwa kumwamini na kumchagua na katika uchaguzi mkuu na kuwa mbunge halali wa Jimbo la Kibiti .

Katika ziara hiyo Mhe. Mbunge  aliambatana na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali  ambayo itahitimishwa katika Kata ya Msala  na huko atakua mgeni rasmi katika mkesha wa sikukuu ya Maulid itakayofanyika tar 16 mwezi huu.

Akiwa katika Kata ya Kiongoroni Tarafa ya Mbwera Mhe. Mbunge amewashukuru wananchi na kuwaahidi kuwatumikia Kwa nguvu zake zote Kwa kusikiliza na kutatua kero mbalimbali za wananchi .

Mpembenue  ametoa mifuko 100 ya saruji Kwa ajili ya ujenzi wa shule shikizi katika kijiji cha King’ongo, mifuko 70 Kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya chama ya kata katika kijiji cha Jaja, mifuko 50 Kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi Kiongoroni na Mifuko 50 Kwa ajili ya shule shikizi Pombwe na kiasi cha shilingi laki moja na nusu (150,000/=) Pamoja na shilingi milioni moja (1,000,000/=) kwa ajili ya ukarabati mdogo wa Zahanati na shule ya msingi pombwe.

Pia ametoa sh. Laki 2 Kwa ajili ya chakula cha wanafunzi wanaofanya  mtihani wa kumaliza kidato cha nne katika sekondari ya Mtanga delta na akaahidi kutoa bati 35 katika makao makuu ya Kata ya Kiongoroni Kwa ajili ya ukarabati wa nyumba ya Mwalimu huku akisisitiza wananchi Kuwa na  tabia ya kujitolea katika shughuli za maendeleo.

Akijibu kero za wananchi katika Kata hiyo Mpembenue amewasihi wananchi kuendelea kuwa watulivu  na kulinda amani hususani katika swala la wafugaji kwani jambo hilo linafanyiwa kazi katika ngazi ya Taifa na kuahidi kuwa changamoto zote amezibeba na anaendelea kuzifanyia kazi.

Vilevile Mbunge  amemshukuru Mhe. Rais Samia Suhuhu Hassan Kwa namna anavyoendelea kutoa fedha za Maendeleo ya ujenzi shule barabara na miundombinu ya umeme ambapo mpaka sasa nguzo za umeme zimekwishafika katika Kata hiyo kwani kazi yake  ni kusikiliza na kuwasilisha kero za wananchi wake na kuhakikisha zinatatuliwa.

Aidha amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kibiti Mohamed Mavura Kwa namna anavyoshirikiana nae kuhakikisha  maendeleo yanapatikana huku  akiwasihi wananchi kushirikiana nae bega Kwa bega Ili Kibiti iweze kusonga mbele.

Kwa nyakati tofauti Mwenyekiti wa Kijiji Cha Kiongoroni na Ruma wamemwomba Mhe.Mbunge kuwa na tabia ya kuwatembelea Ili kujenga Imani Kwa wananchi waliomchagua kwani kiu yao ilikuwa ni kuonana nae .

Nae Diwani wa Kata ya Kiongoroni Mhe. Muharami Tota, amesema amefurahishwa na kufarijika na ugeni wa Mhe. Mbunge na viongozi aliambatana nao, kwani umejibu maswali mengi aliyokua akiulizwa na wananchi wa Kata hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.