• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • Maswali na majibu
    • Barua pepe
KIBITI DISTRICT COUNCIL
KIBITI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mazingira
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo na Umwagiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Nyuki
      • Uchaguzi na Utawala Bora
  • Fursa za Uwekezaji
    • Ufugaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Vivutio vya utalii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Sheria
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Mifumo

ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA KIBITI KATIKA KATA YA KIONGORONI.

Posted on: August 23rd, 2024

21.08.2024

Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo akiwa ameambatana na Katibu Tawala Bi. Maria Katemana amefanya ziara katika Kata ya Kiongoroni kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi sambamba na kukagua miradi ya maendeleo.

Akiwa katika Kitongoji cha King'ongo Kanali Kolombo amekagua ujenzi wa shule Shikizi King'ongo yenye jumla ya madarasa matatu na Ofisi moja ya walimu inayojengwa kwa mchango wa Mhe. Mbunge na nguvu za Wananchi ambapo ameahidi kuhakikisha Serikali inamalizia hatua iliyobakia.

Vilevile ametembelea shule ya Sekondari ya Mtanga Delta ambapo jengo la nyumba ya walimu iliharibiwa na kimbunga Hidaya pia alitembelea  Zahanati ya Mtanga Delta na kubaini changamoto zilizopo kama ukosefu wa umeme, maji safi ya uhakika, makazi ya watumishi pamoja na uhitaji wa zahanati hiyo kurejeshwa katika hadhi yake ya kuwa Kituo cha Afya.

Pia Kanali Kolombo ametembelea Zahanati ya Ruma pamoja na Shule ya Msingi  Ruma pamoja na Shule ya Msingi Kiongoroni iliyopo katika makao makuu ya Kata  ambapo aliwataka watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii wakati changamoto walizonazo zikitafutiwa ufumbuzi na kisha akazungumza na  Wananchi ili kusikiliza kero ama changamoto zilizopo kijijini hapo.

Akijibu kero za Wananchi Kanali Kolombo ameziagiza Taasisi zote zinazoshughulikia masuala ya maji, umeme, vitambulisho vya Taifa ( NIDA ) na Vyeti vya vizazi na vifo (RITA) kuweka  kambi katika maeneo hayo ili kuhakikisha huduma hizo zinapatikana kwa wananchi hao huku akisisistiza mkandarasi wa Barabara kukamilisha Ujenzi wa Barabara ya kutoka Mtanga Delta mpaka Ruma kwa muda uliopangwa.

Kuhusu suala la Mifugo Kanali Kolombo   amesema tayari wamekwishaanza Operesheni ambayo itakuwa endelevu huku akisisitiza kila mfugaji kuwa na kitalu cha kufugia Mifugo yake kwa kufuata utaratibu  kwani itasaidia kumaliza migogoro ya mwingiliano wa malisho na mashamba ya wakulima.

Kwa upande wa elimu amewataka wakazi Kata ya Kiongoroni kuhakikisha wanawapeleka watoto wao shule na kuwataka walimu kuongeza jitihada za  kufundisha kwa kushindanisha shule ili kwa kusudio la kupandisha ufaulu ambao umekuwa ni changamoto kubwa katika Wilaya hiyo.

Aidha ameahidi kuchangia Sh. 600,000 kwa ajili ya ujenzi wa kivuko kitakachounganisha Kitongoji cha Bweni na Kijiji cha Kiongoroni na Sh. 200,000 kwa ajili ya ukamilishwaji wa shule ya Madrasa Kitongoji cha Bweni. Mbali na ahadi hizo amemuagiza Mkurugenzi kuhakikisha Ujenzi wa shule shikizi King'ongo unakamilika pamoja na kuwapelekea samani na ubao ili watoto wakasome katika Mazingira mazuri. 

Mwisho Diwani wa Kata hiyo Mhe. Muharami Tota alimshukuru Mkuu huyo wa Wilaya kwa ujio wake akisema kwao imekuwa ni siku ya kipekee yenye furaha kubwa katika historia ya Wanakiongoroni.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MAENEO YA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBITI September 16, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI BODI YA ELIMU April 04, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA February 26, 2024
  • MWALIKO WA WATAZAMAJI February 16, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KIBITI YAPOKEA CHANJO YA MIFUGO.

    May 08, 2025
  • JAJA KUFAIDIKA NA UTALII IKOLOJIA KUPITIA FUKWE .

    May 06, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA WILAYANI KIBITI NA KUTEMBELEA MIRADI 13

    April 08, 2025
  • WANAWAKE KIBITI WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI LEO.

    March 06, 2025
  • Angalia Vyote

Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa

More Videos

Kurasa za Haraka

  • Ajira
  • Madiwa wa sasa
  • Barua pepe
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Maswali na Majibu
  • Fursa za Uwekezaji
  • Maktaba ya Picha
  • Fomu Mbalimbali
  • Facebook: kibitidc

Tovuti zinazoshabiana

  • TANZANIA GOVERNMENT PORTAL
  • COAST REGION WEBSITE
  • TAMISEMI
  • PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE MANAGEMENT AND GOOD GOVERNANCE
  • NECTA
  • TOVUTI YA AJIRA
  • IKULU
  • TANZANIA BUREAU OF STATISTIJS
  • Tume ya uchaguzi Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibiti

   

    • Sera binafsi
    • Kanusho
    • Maswali na majibu
    • Sitemap
    • Huduma zetu

Copyright ©DED-KIBITI 2017 . All rights reserved.